jaridahuru
https://jaridahuru.blogspot.com/2014/09/teknolojia-tamesco-yawaondoa-wananchi.html
SHIRIKA la Ugavi wa Umeme nchini (Tanesco), limesema mgodi wa kufua
umeme uliojengwa Kidatu Morogoro mwaka 1975, bado una uwezo wa kuzalisha
nishati hiyo kwa kiwango cha kutosha.
Kauli hiyo, ilitolewa juzi na Meneja wa Mgodi huo, Injinia Joseph
Lyaruu, wakati wa ziara ya wandishi wa habari nchini, kujionea kazi
zinavyofanyika katika mgodi huo.
Alisema uwezo huo ulitokana na jitihada za Tanesco kuendelea
kuuboresha hatua kwa hatua, ambako hivi sasa katika mgodi huo kumefugwa
mashine nne ikilinganishwa na awamu ya kwanza ulipojengwa, ambazo zina
uwezo wa kuzalisha umema kwa ufanisi mkubwa ambao unakwenda sambamba na
ongezeko la wateja kila mwaka.
“Sio kweli kama mtambo hauwezi kuzalisha umeme kama inavyodhaniwa na
baadhi ya watu, bado unao uwezo wa kufanya kazi katika kipindi cha miaka
50, hata nchini India iko mitambo ambayo imefanya kazi zaidi ya miaka
50,” alisema Injinia Lyaruu.
Lyaruu, alisema Watanzania hawana haja ya kuwa na wasiwasi kuhusu
uzalishaji katika mgodi huo, kwa sababu shirika kwa kushirikiana na
wahisani wako katika mkakati kubadili baadhi ya vifaa ambavyo vimekuwepo
tangu unajengwa.
Akizungumzia kuhusu hali ya maji, Lyaruu alisema Watanzania watarajie
kupata huduma hiyo kwa ufanisi na bila kikomo, kwa sababu kipindi hiki
maji ya kutosha yapo.
Alizitaja baadhi ya changamoto zinazowakabili kuwa ni uhaba wa maji,
shughuli za kibinadamu karibu na mito inayoingia kwenye mabwawa na
uchepushaji wa maji kwa ajili ya kilimo na shughuli nyingine.
Naye Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali watu, Rashid Msingwa, alisema
mgodi huo una wafanyakazi 104, ambao wanafanya kazi mbalimbali ikiwemo
utoaji wa huduma za jamii.
Related
TEKNOLOJIA: TUME YA UCHAGUZI 'NEC' YAENDELEZA UTATA ZABUNI YA MASHINE ZA KUPIGIA KURA 'BVR'
TUME ya Taifa ya Uchaguzi nchini (NEC), imezidi kuibua utata kuhusiana na gharama halisi za kupata mzabuni wa kuboresha daftari la kudumu la kupigia kura kwa njia ya kielektroniki, (BVR), ba...
TEKNOLOJIA: JE UNAFAHAMU KAMA TAARIFA ZAKO ZA MATUMIZI YA SIMU ZIKO SALAMA? JE MITANDAO YA SIMU INA USIRI?
Ukikutana na Watanzania 10 angalau nusu yao watakuwa na kifaa au vifaa vya mawasiliano kama simu na kompyuta. Vifaa hivi vimesajiliwa kwa majina yao na taarifa zao nyingine ambazo zinawez...
TEKNOLOJIA: TCRA YAONYA WANAOWADHALILISHA WENZAO KWENYE MTANDAO, YAAHIDI KUWAFIKISHA MAHAKAMANI
MAMLAKA ya mawasiliano nchini ,TCRA, imewaonya wale wote wanaotumia mitando kuchafua na kudhalilisha watu waache mara moja vinginevyo watakabiliwa na mkono wa sheria. Onyo hilo limet...
Post a Comment

:noprob:

:smile:

:shy:

:trope:

:sneered:

:happy:

:escort:

:rapt:

:love:

:heart:

:angry:

:hate:

:sad:

:sigh:

:disappointed:

:cry:

:fear:

:surprise:

:unbelieve:

:shit:

:like:

:dislike:

:clap:

:cuff:

:fist:

:ok:

:file:

:link:

:place:

:contact:
Tabs
Za JuuMitandaoPiga Kura
Za Juu
-
Mmoja wa waasisi wa mtandao wa kijamii wa Instagram, amesema kuwa sheria zake kuhusu picha za uchi hazimbagui mtu yeyote. Kampuni hi...
-
Dar es Salaam. Harakati za kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2015 zimeanza. Polisi wameanza mafunzo yatakayowaongezea uwezo wa kusimamia uchagu...
-
AMA kweli kufa kufaana! Lile bifu zito lililokuwa likitokota kati ya wapendwa wawili, Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu na mwi...








