jaridahuru

Mitandao

TEKNOLOJIA: TUME YA UCHAGUZI 'NEC' YAENDELEZA UTATA ZABUNI YA MASHINE ZA KUPIGIA KURA 'BVR'


TUME ya Taifa ya Uchaguzi nchini (NEC), imezidi kuibua utata kuhusiana na gharama halisi za kupata mzabuni wa kuboresha daftari la kudumu la kupigia kura kwa njia ya kielektroniki, (BVR), baada ya kudai gharama zilizotajwa katika hukumu ya mamlaka ya ununuzi wa umma (PPAA), si sahihi.

Hivi karibuni, PPAA iliweka katika tovuti yake uamuzi wa kesi namba 33/2013-14, kuihalalisha kampuni ya Ms Lithotec kuwa mzabuni halali katika ukamilishaji wa vifaa vya kupigia kura kielektroniki na kuonyesha gharama alizopewa mzabuni huyo ni dola 117,184,507.05 za Marekani.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar esSalaam jana, Mkurugenzi wa NEC, Julius Mallaba, alisema, fedha halali walizokubaliana na kampuni ya Lithotec kukamilisha mchakato wote ni dola 89,094,407.05 huku gharama za BVR peke yake ikiwa ni dola 71,032,500 za Marekani.

Mallaba alisema, kabla ya mkataba huo kusainiwa kati ya NEC na Ms Lithotec, mmoja wa wazabuni MS/Morpho alilalamikia  zabuni hiyo PPAA, hali iliyowafanya wapeleke makubaliano ya awali katika mamlaka hiyo.

“Naomba ieleweke, gharama zinazotajwa sijui dola milioni 117 sisi hatuzijui, sisi tuna gharama zetu halisi katika mkataba tofauti na zinazoandikwa,” alisema Mallaba.

Kampuni ya MS Lithotec, imefanikiwa kupata zabuni hiyo baada ya kuitishwa kwa mara ya pili kutokana na uamuzi wa PPAA kuitaka NEC ianze mchakato huo upya, baada ya malalamiko ya wazabuni wengine.

Related

Technolojia 7862232838845945760

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item