jaridahuru

Mitandao

SOKA: LIVERPOOL YAANZA KUONESHA MAKALI YA MSIMU UJAO, YACHABANGA BORUSIA 4:0

Liverpool inajianda kwa msimu mpya wa ligi ya Uingereza
Mshambulizi wa Liverpool Dejan Lovren aliifungia the Reds bao lake la kwanza katika mechi yake ya kwanza Liverpool ilipoilaza Borussia Dortmund mabao 4-0 katika mechi ya kirafiki.
Daniel Sturridge ndiye aliyeifungua kivuno hicho cha mabao baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Phillippe Coutinho.
Lovren, aliyejiunga na ''the Reds'' akitokea Southampton, katika kandarasi ya pauni milioni 20m alifuma bao la pili kwa kichwa alipotumia vyema kona kutoka kwa Steven Gerrard .
Liverpool inajianda kwa msimu mpya wa ligi ya Uingereza
Jordan Henderson alikamilisha kivuno hicho baada ya kufaidi pasi ya Sturridge.
Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers aliwachezesha wachezaji wapya Lovren, Javier Manquillo, Emre Can Rickie Lambert katika mechi hiyo.
Liverpool, itafungua kampeini ya msimu huu dhidi ya Southampton jumapili ijayo.
Kocha Rodgers aliwachezesha wachezaji wapya
Kwa upande wao Dortmund ilikuwa inatumia mechi hiyo kujiandaa kwa mechi dhidi ya Bayern Munich ya kuwania kombe la German Super Cup siku ya jumatano.
Dortmund itafungua kampeini yake dhidi ya Bayer Leverkusen tarehe 23 Agosti.

Related

Worldcup 2014 1137091553180065053

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item