jaridahuru

Mitandao

VYUONI: TAHLISO YADAI SH. 1.6 BILIONI HAZIJALIPWA VYUONI, YASEMA ITATUMIA NJIA MBADALA IWAPO WIZARA HAITATOA TAMKO


Dar es Salaam. Jumuiya ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Tanzania (Tahliso) imetoa wiki moja kwa Serikali kutoa majibu ya lini vyuo saba vitapatiwa fedha kwa ajili ya wanafunzi wanaokwenda kwenye mafunzo kwa njia ya vitendo.

Jumuiya hiyo imesema kama wizara husika itashindwa kutoa tamko lolote kuhusu fedha hizo, Tahliso itafanya uamuzi mwingine kuwakomboa wenzao waweze kuendelea na mafunzo ya vitendo kama ratiba inavyoonyesha.

Akizunguza na waandishi wa habari jana jijini hapa, mwenyekiti wa jumuiya hiyo, Musa Mdede alisema wiki nne zimepita tangu mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi yaanze, lakini bado vyuo saba havijapata pesa.

Vyuo ambavyo havijapata pesa hadi sasa ni Saut tawi la Mwanza na Tabora, Tumaini Makumira Arusha, Stephano, Moshi mkoani Kilimanjaro, Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Teophilo Kisanji, Mbeya na Chuo Kikuu cha Jordan, Morogoro. Fedha zinazotakiwa ni Sh1.6 bilioni.
“Tunataka Serikali itueleze kwanini baadhi ya vyuo havijapewa pesa hadi sasa wakati mafunzo yameshaanza,” alisema Mdee.

Mkurugenzi wa habari wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Tanzania (HESLB), Cosmas Mwaisoba hakuweza kupatikana jana kuzungumzia suala hilo.

Katika hatua nyingine, Tahliso imewaonya wanasiasa wanaoingilia masuala ya elimu kupitia umoja wao kwa lengo la kujinufaisha, kuacha tabia hiyo mara moja.

“Jumuiya yetu ipo kwa ajili ya kutetea masilahi ya wanafunzi na siyo masilahi ya chama chochote cha siasa. Nawaomba wanasiasi wajiepushe kujiingiza kwenye umoja wetu kwa vile hawatafaidika na chochote,” alisema.

“Natoa onyo kwa wanasiasa. Hakuna sababu kwa wao kuingilia kati utendaji wa Tahliso, kwani dhamira yetu siyo kujiingiza kwenye siasa ila kutetea haki za wanafunzi nchini,” aliongeza

Related

VYUONI: SERA YA KUDHIBITI MAVAZI VYUONI YATUNGWA, WATAKAO KAIDI KUCHUKULIWA SHERIA KALI

SERA ya kudhibiti mavazi yasiyoendana na maadili, yanayovaliwa na wanafunzi wa vyuo vikuu hapa nchini, inaelezwa itakuwa muarobaini kwa wanafunzi husika. Akizungumza na waandishi wa habari ...

VYUONI: CHUO CHA BAHARI DAR ES SALAAM (DMI) CHAPATA BAHATI YA KUTEMBELEWA NA N/WAZIRI WA UCHUKUZI

Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya Mkuu wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), mara baaada ya kuwasili chuoni hapo kuangalia shug...

VYUONI: MBUNGE WA CHALINZE, RIDHIWANI KIKWETE AKABIDHI SEKONDARI VITANDA 267

MBUNGE wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete, amekabidhi vitanda 267 katika shule za sekondari za bweni saba jimboni humo vyenye thamani ya sh milioni 53.4.  Akizungumza wakati wa kukabidhi v...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item