jaridahuru

Mitandao

VYUONI: TAHLISO YADAI SH. 1.6 BILIONI HAZIJALIPWA VYUONI, YASEMA ITATUMIA NJIA MBADALA IWAPO WIZARA HAITATOA TAMKO


Dar es Salaam. Jumuiya ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Tanzania (Tahliso) imetoa wiki moja kwa Serikali kutoa majibu ya lini vyuo saba vitapatiwa fedha kwa ajili ya wanafunzi wanaokwenda kwenye mafunzo kwa njia ya vitendo.

Jumuiya hiyo imesema kama wizara husika itashindwa kutoa tamko lolote kuhusu fedha hizo, Tahliso itafanya uamuzi mwingine kuwakomboa wenzao waweze kuendelea na mafunzo ya vitendo kama ratiba inavyoonyesha.

Akizunguza na waandishi wa habari jana jijini hapa, mwenyekiti wa jumuiya hiyo, Musa Mdede alisema wiki nne zimepita tangu mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi yaanze, lakini bado vyuo saba havijapata pesa.

Vyuo ambavyo havijapata pesa hadi sasa ni Saut tawi la Mwanza na Tabora, Tumaini Makumira Arusha, Stephano, Moshi mkoani Kilimanjaro, Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Teophilo Kisanji, Mbeya na Chuo Kikuu cha Jordan, Morogoro. Fedha zinazotakiwa ni Sh1.6 bilioni.
“Tunataka Serikali itueleze kwanini baadhi ya vyuo havijapewa pesa hadi sasa wakati mafunzo yameshaanza,” alisema Mdee.

Mkurugenzi wa habari wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu Tanzania (HESLB), Cosmas Mwaisoba hakuweza kupatikana jana kuzungumzia suala hilo.

Katika hatua nyingine, Tahliso imewaonya wanasiasa wanaoingilia masuala ya elimu kupitia umoja wao kwa lengo la kujinufaisha, kuacha tabia hiyo mara moja.

“Jumuiya yetu ipo kwa ajili ya kutetea masilahi ya wanafunzi na siyo masilahi ya chama chochote cha siasa. Nawaomba wanasiasi wajiepushe kujiingiza kwenye umoja wetu kwa vile hawatafaidika na chochote,” alisema.

“Natoa onyo kwa wanasiasa. Hakuna sababu kwa wao kuingilia kati utendaji wa Tahliso, kwani dhamira yetu siyo kujiingiza kwenye siasa ila kutetea haki za wanafunzi nchini,” aliongeza

Related

VYUONI: UCHAFU WANAOFANYA WADADA VYUONI, JE WAZAZI WANAWAFAHAMU BINTI ZAO?

Katika siku za hivi karibuniwanafunzi hasa wa vyuo vikuu wamekuwa na tabia chafu ya kujirekodi wakiwawanafanya mapenzi, na kupiga picha za utupu nakuziweka katika mitandao ya kijamiii. Hatuweza k...

JH AJIRA: UN WAMETANGAZA NAFASI YA 'ICT ASSOCIATE' SIO LAZIMA UWE NA DIGRII.

ICT ASSOCIATE POSITION DESCRIPTION: From the Daily News of 20th MayUNDP Tanzania Office wishes to recruit a suitable Tanzania national to fill ICT Associate position. Location: Dar es Salaa...

VYUONI: MWANAFUNZI WA SAUT MWANZA APIGWA NA WENZAKE HADI KIFO KWA KUHISIWA KUWA MWIZI

Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agustino (SAUT) cha jijini hapa, Helma Michael (22)  ameuawa kwa kupigwa mawe na wanafunzi wenzake, wakimhisi kuwa ni mwizi wa kompyuta ndogo za mkononi...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item