jaridahuru

Mitandao

ELIMU: MSHINDI WA TAJI LA MISS TZ 2012, BRIGITTE ALFRED, JAT KUWASOMESHA ALBINO 50 NCHINI




WALEMAVUwa ngozi (Albino) 50 wanatarajiwa kupewa mafunzo ya ujasiriamali kuanzia Agosti 18, jijini Dar es Salaam.

Mafunzo hayo yanaratibiwa na Taasisi ya Brigitte Alfred Foundation (BAF) inayomilikiwa na aliyekuwa Miss Tanzania 2012, Brigitte Alfred kwa kushirikiana na Taasisi ya Junior Achievement Tanzania (JAT).

Akizungumza katika uzinduzi wa programu hiyo uliofanyika jana, Brigitte alisema mafunzo hayo yanalenga namna ya kujitambua, kutathmini aina mbalimbali za biashara, kutunza pesa, kuandika mchanganuo wa biashara, kutembelea sehemu mbalimbali zinazoendana na biashara na jinsi ya kuanza biashara.

“Mafunzo haya yatachukua muda wa mwaka mmoja, kila mshiriki wa mafunzo haya atapatiwa kitabu chenye masomo yote ili aweze kuendelea kujisomea,” alisema Brigitte.

Mkurugenzi wa JAT, Maria Ngowi alisema kuwa wamejipanga kufanikisha mpango huo na wanaamini watakaopata mafunzo hayo watafanikiwa katika maisha yao.

Alisema JAT imejikita katika nyanja tatu ambazo ni ujasiriamali, elimu ya kuzalisha, kuwekeza na kutunza fedha na elimu ya kazi.

Ngowi alisema JAT ni sehemu ya taasisi kubwa ulimwenguni ya Junior Achievement International, ambayo iko katika nchi 120 duniani huku Afrika ikiwa katika nchi 17.

Related

BREAKING NEWS: BOMU LARUSHWA NDANI YA BASI KIGOMA-TZ WATU WAUAWA WENGINE WAJERUHIWA. ANGALIA HAPA

Kigoma. Watu watatu wamekufa akiwepo mtoto mchanga na wengine sita kujeruhiwa baada ya basi dogo la abiria (Hiace) kurushiwa bomu na watu wasiojulikana huko Kasesema, Kigoma alfajiri ya leo. ...

KIMATAIFA: SERIKALI YA LIBERIA YAANZA KUWATAFUTA WAGONJWA WA EBOLA WALIOTOROKA KAMBINI

  Kituo kilichotengwa na kuwekewa karantini kwa sababu ya ebola, kimeshambuliwa na zana kuporwa katika mji mkuu wa Liberia, Monrovia. Watu kama 20 hadi 30 waliowekwa hapo kuangaliwa ka...

KITAIFA: WAHAMIAJI HARAMU TOKA SOMALIA WAKAMATWA MAKAMBAKO IRINGA WAKIWA NDANI YA ROLI LA SARUJI

  IDARA ya Uhamiaji mkoani hapa, imewakamata wahamiaji haramu 21 kutoka nchi ya Ethiopia walioingia nchini kwa kutumia roli la kubebea saruji katika eneo Mashujaa mjini Makambako. Naibu Kamish...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item