jaridahuru

Mitandao

KITAIFA: WAHAMIAJI HARAMU TOKA SOMALIA WAKAMATWA MAKAMBAKO IRINGA WAKIWA NDANI YA ROLI LA SARUJI

 
IDARA ya Uhamiaji mkoani hapa, imewakamata wahamiaji haramu 21 kutoka nchi ya Ethiopia walioingia nchini kwa kutumia roli la kubebea saruji katika eneo Mashujaa mjini Makambako.

Naibu Kamishna wa Idara ya Uhamiaji, Rose Mhagama alisema wahamiaji hao walikamatwa Agosti 14, mwaka huu, saa 12:30 jioni wakati kikosi cha uhamiaji kikiwa katika doria.

Mhagama alisema kuwa kikosi hicho kilifanikiwa kubaini lori lililowabeba likitokea Makambako kuelekea Songea lenye namba za usajili T587 CSN likiwa na tela namba T780 CHM lililokuwa likiendeshwa na dereva aliyefahamika kwa jina moja la Nyange.

Alisema lori hilo ni mali ya Everest Flight LTD, ambapo baada ya dereva huyo kukaguliwa alieleza kuwa alikuwa akiwasafirisha kuelekea nchini Malawi.

“Dereva alipohojiwa alisema alikuwa anakwenda kukutana na mtu ambaye anahusika na watu hao akiwa mjini Njombe, ili aweze kuwashusha pale Njombe na waweze kuendelea na utaratibu wao wa kwenda Malawi,”alisema.

Mhagama alieleza kuwa jeshi la polisi linamsaka dereva huyo baada ya kutoroka na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano wa kuwafichua wahamiaji haramu.

Related

Kitaifa 2712025448654268552

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item