jaridahuru

Mitandao

AFYA: DAKTARI ALIYEMTIBU MGONJWA WA EBOLA NIGERIA AAMBUKIZWA UNGONJWA HUO HATARI

Daktari aliyemtibu mgonjwa wa Ebola ameabukizwa nchini Nigeria 

Daktari mmoja jijini Lagos Nigeria aliyemtibu mgonjwa aliyefariki kutokana na homa ya Ebola amepatikana ameambukizwa na maradhi hayo.

Daktari huyo ambaye alimtibu mfanyikazi wa wizara ya hazina nchini Liberia aliyepatikana na homa hiyo ya Ebola na kuwa mtu wa kwanza kuaga dunia nchini Nigeria sasa amedhibitishwa kuambukizwa .

Waziri wa afya nchini humo Onyebuchi Chukwu amesema kuwa daktari huyo pamoja na watu wengine 70 waliokutana na marehemu wametengwa kwa uchunguzi na matibabu zaidi.

Mataifa yaliyoathirika na homa ya Ebola

Patrick Sawyer alitua nchini Nigeria Julai tarehe 20 na akafa tarehe 25 katika hospitali moja mjini Lagos.

Mlipuko huu wa ugonjwa wa ebola katika ukanda wa magharibi mwa Afrika umesababisha vifo vya watu zaidi ya 826 katika mataifa ya Guinea, Liberia na Sierra Leone.

Related

Jamii 4991433802016558251

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item