AFYA: DAKTARI ALIYEMTIBU MGONJWA WA EBOLA NIGERIA AAMBUKIZWA UNGONJWA HUO HATARI
https://jaridahuru.blogspot.com/2014/08/afya-daktari-aliyemtibu-mgonjwa-wa.html
Daktari mmoja jijini Lagos
Nigeria aliyemtibu mgonjwa aliyefariki kutokana na homa ya Ebola
amepatikana ameambukizwa na maradhi hayo.
Waziri wa afya nchini humo Onyebuchi Chukwu amesema kuwa daktari huyo pamoja na watu wengine 70 waliokutana na marehemu wametengwa kwa uchunguzi na matibabu zaidi.
Mlipuko huu wa ugonjwa wa ebola katika ukanda wa magharibi mwa Afrika umesababisha vifo vya watu zaidi ya 826 katika mataifa ya Guinea, Liberia na Sierra Leone.