jaridahuru

Mitandao

KIMATAIFA: KUNDI LA AL-SHABAAB WATOA AMRI, WATAKA WANAWAKE WAVAE Niqab


Al shabaab

Wanamgambo wa Al-shabaab nchini Somalia wamewakamata takriban wanawake mia moja na kuwaaamuru kuvalia mavazi yanayostahili kwa wanawake wa kiislamu kuambatana na sheria za dini hiyo la sivyo wapate kichapo.

Wanawake hao walikamatwa sokoni katika eneo la Buala karibia kilomita mia tatu Kusini-Magharibi mwa Mogadishu.
Mwandishi wa BBC nchini humo Mohamed Mohamed anasema ni nadra kwa Al-shabaab kuwakamata watu wengi kwa wakati mmoja kama hivyo.

 Baadhi ya wanawake hujifunika gubigubi kutoka kichwani hadi miguuni 

Wanawake hao walikamatwa wakiwa sokoni na kupewa onyo kabla ya kuachiliwa huru.
Hawakuadhibiwa kwa sababu lilikuwa kosa lao la kwanza lakini walionywa kuwa watachapwa hadharani ikiwa wangepatikana na kosa hilo kwa mara nyingine.

Mwandishi wa BBC anasema kuwa wanawake hao walivalia mavazi mapesi na kukosa kujifunika nyuso zao kutokana na joto kali.

Wanawake hao waliamrishwa kuvaa Niqab,vazi linalowafunika mwili mzima huku sehemu ndogo ya uso ikiachwa nje ili kuwawezesha kuona.

Jina al shabaab linalo maanisha "vijana" kwa kiarabu,linapigania mfumo wa kiislamu wa wahhabi saudia.

Watu ambao washawahi kupatikana na kosa la Zinaa wamepigwa mawe hadi kufa na wezi kukatwa mikono.

Serikali ya Somalia inayofadhiliwa na umoja wa mataifa,ikisaidiwa na wanajeshi wa Muungano wa Afrika, imefaulu kutimua Al-shabaab nje ya miji mikubwa nchini humo lakini kundi hilo bado linaendelea kutekeleza mashambulizi huko.

Related

KIMATAIFA: KENYATTA AKALIA KUTI KAVU, SHAMBULIO LINGINE LAUA 20 HUKO WAJIR KENYA

Kuna taarifa kuwa watu ishirini wameuawa katika shambulio kwenye kijiji Mashariki Kaskazini mwa Kenya. Mwandishi wa BBC anasema watu wenye silaha walivamia kijiji cha Gunana katika County ya Waj...

KIMATAIFA: WAPIGANAJI WA JIHAD WAENDELEA KUTEKA MIJI ZAIDI

Wapiganaji wa Jihadi wameendelea kuyateka maeneo zaidi nchini Iraq,baada ya kuliteka eneo moja la kivuko karibu na mpaka wa Syria, na sasa wanalekea mjini Baghdad kupitia bonde la Euphrates. Mw...

KIMATAIFA: KITUO CHA NTV UGANDA KIMEFUNGIWA BAADA YA KUMUONESHA MUSEVENI AKIWA AMESINZIA BUNGENI

Serikali ya Uganda imekifungia kituo kikubwa cha Televisheni cha nchi hiyo NTV kuripoti habari zozote zinazomhusu Rais baada ya kurusha hewani picha zinazomuonyesha Rais Yoweri Museveni amesinzia ...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item