jaridahuru

Mitandao

KIMATAIFA: KITUO CHA NTV UGANDA KIMEFUNGIWA BAADA YA KUMUONESHA MUSEVENI AKIWA AMESINZIA BUNGENI

Serikali ya Uganda imekifungia kituo kikubwa cha Televisheni cha nchi hiyo NTV kuripoti habari zozote zinazomhusu Rais baada ya kurusha hewani picha zinazomuonyesha Rais Yoweri Museveni amesinzia bungeni.
 
Mkurugenzi wa kituo cha habari za serikali Dennis Katungi amenukuliwa akisema: “Rais ana tabia zake wengi mnajua, huwa anatafakari na wanajua lakini bado wameonyesha picha hizo na kusema alikuwa amesinzia.”
 
Msemaji wa serikali Ofwono Opondo amethibitisha kuwa NTV Uganda itachukuliwa hatua za kinidhamu ambapo wameifungia kuripoti habari zozote zinazomhusu rais wakati bado serikali ikiangalia uhusiano wake na chombo hicho.
Museveni
Rais Yoweri Museveni
 
Ameituhumu NTV kwa kukosa utaalamu wa uandishi na kuegemea upande mmoja lakini hata hivyo hatua hiyo si ya kudumu ni ya muda tu kuwafanya wafikirie upya.

Related

Kimataifa 2690636586008675065

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item