jaridahuru

Mitandao

ELIMU: MITIHANI YA SHULE YA MSINGI KUSAHIHISHWA KWA KUTUMIA COMPUTER (OMR) ILI KUDHIBITI UDANGANYIFU


KATIKA kutekeleza majukumu yake ikiwemo Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limepata mafanikio  mbalimbali kuboresha Mfumo wa Usahihishaji wa Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE) na kupanga shule kulingana na kiwango cha ufaulu “Ranking” kwa kuonesha shule zilizofanya vizuri na shule ambazo hazikufanya vizuri. 

NECTA ni taasisi ya umma chini ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ambayo ilianzishwa Mwaka 1973. 

Kaimu Katibu Mtendaji wa NECTA Dk. Charles Msonde, anasema mafanikio mengine ni kudhibiti udanganyifu katika mitihani, matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano(TEHAMA) katika usajili wa watahiniwa, kuweka picha ya mtahiniwa husika kwenye cheti  na  kujenga kituo cha usahihishaji Mbezi Wani.

Akizungumza kwa kina anasema kuanzia mwaka 2012 watahiniwa wa Kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE) walianza kufanya mtihani wa kutumia karatasi maalum za (OMR) ambazo husahihishwa kwa kutumia mfumo wa kompyuta. 

Mfumo huo anasema umekuwa na manufaa ikilinganishwa na usahihishaji wa mkono. Anabainisha kuwa kwa kutumia mfumo wa OMR, idadi ya watahini na siku za kusahihisha Mtihani zimepungua na hivyo kupunguza gharama za usahihishaji.

 “Mtihani wa mwaka 2013 jumla ya watahini 301 walishirki katika zoezi la usahihishaji ikilinganishwa na idadi ya watahini zaidi ya 4000 ambao walikuwa wakishiriki kabla ya mfumo wa usahihishaji wa kompyuta haujaanza. Usahihishaji huo ulifanyika kwa siku 16 badala ya siku 30 zilizokuwa zikitumika awali. Pia usahihishaji ulifanyika kwa usahihi zaidi ikilinganishwa na usahihishaji wa kalamu unaofanywa kwa mkono. 

“Ili usahihishaji wa kutumia mkono uwe sahihi, miaka ya nyuma Baraza la Mitihani lililazimika kuwa na hatua nyingi za uhakiki ili kuepusha kuwepo kwa makosa machache ya kibinadamu, jambo ambalo lilifanya kazi ya usahihishaji kutumia muda mrefu, watu wengi na gharama kubwa.

“Tumewahi kulinganisha kati ya wasahihishaji wa mkono na Mfumo wa Kompyuta ambapo ilithibitika kuwa  Mfumo wa Kompyuta husahihisha kwa usahihi wa asilimia mia moja wakati msahihishaji wa mkono aliweza kufanya makosa ya kibinadamu katika zoezi hilo  na hivyo kufanya kazi ya usahihishaji kuwa na hatua nyingi za uhakiki katika kuondoa dosari zinazobainika,” anasema.
Dk. Msonde anaedelea kueleza kuwa  baada ya kuanza kutumia mfumo wa OMR na kusahihisha kwa kutumia kompyuta, Baraza la Mitihani limeweza kufanya uchambuzi kuonesha namna watahiniwa wanavyojibu maswali kwa kubainisha maswali waliyopata, waliyokosa, majibu waliyojaza na namna walivyoelewa maswali ya mitihani.

Anasema uchambuzi huo wa kitaalam umeandaliwa na kuchapwa katika vitabu maalum ambavyo vinasambazwa katika shule zote ili kuwawezesha walimu kujua namna ya kuwasaidia wanafunzi katika kujibu maswali ipasavyo. Hii itasaidia kuboresha ufaulu wa watahiniwa katika mitihani ijayo.

Dk. Msonde anasema baraza limefanikiwa kupanga  shule katika makundi mbalimbali ya ufaulu na kufafanua uwezo wa kila kundi. Taarifa hii imewekwa katika tovuti za Baraza la Mitihani la Tanzania, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Ofisi ya waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) na itawawezesha wadau mbalimbali wa elimu kufanya maamuzi yenye lengo la kuboresha elimu kwa kila shule kulingana na uwezo uliooneshwa.

Anafafanua kuwa taarifa hii itasaidia Serikali katika kupima mafanikio yaliyopatikana kwa kila shule kwa kulinganisha na uwekezaji wa rasilimali kwa kipindi husika.

Kwa mujibu wa  maelezo ya Kaimu Katibu Mtendaji, NECTA kwa kushirikiana na Kamati za Uendeshaji Mitihani  katika ngazi za Mikoa, Wilaya na Wasamaria wema, limeweza kwa kiasi kikubwa kudhibiti udanganyifu katika Mitihani.

Dk. Msonde anatoa mfano katika Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi mwaka 2013 watahiniwa waliofutiwa matokeo kwa kufanya udanganyifu walikuwa 13 tu idadi ambayo ni ndogo ikilinganishwa na watahiniwa 9,736 waliobainika kufanya udanganyifu mwaka 2011 na 293 mwaka 2012.

Katika mtihani wa kumaliza kidato cha nne mwaka 2013; anasema watahiniwa waliofutiwa matokeo kwa kufanya udanganyifu walikuwa 272 ikilinganishwa na 789 mwaka 2012 na 3,303 mwaka 2011.
“Katika  mtihani wa kumaliza kidato cha sita mwaka 2013 mtahiniwa mmoja tu ndiye aliyefutiwa matokeo.  Idadi hii ni ndogo ikilinganishwa na watahiniwa watano  waliobainika kufanya udanganyifu mwaka 2011 na watatu mwaka 2012,” anaeleza Dk. Msonde.

Dk. Msonde anasema baraza linafanya usajili wa watahiniwa kwa kutumia mfumo wa kompyuta ambapo taarifa  za watahiniwa wa shule hukusanywa kwa kushirikiana na  Mkuu wa Shule na kuhifadhiwa katika CD ambayo huwasilishwa NECTA.  Pia watahiniwa wa kujitegemea hujisajili wenyewe kwa kutumia mtandao.

Dk. Msonde anasema miaka ya nyuma watu wengi walikuwa wanatumia vyeti vya watu wengine au kughushi vyeti.  Kuanzia mwaka 2008/2009 NECTA ilianza utaratibu wa kuweka picha ya mtahiniwa husika kwenye cheti chake. Mafanikio haya yamelifanya Baraza kuwa na uwezo wa kuwabaini na kuwachukulia hatua watahiniwa wanaoghushi vyeti au kutumia vyeti vya watu wengine.

Anasema kazi ya usahihishaji Mitihani hufanyika katika vituo mbalimbali. Mwaka 2010 Baraza la Mitihani lilikamilisha ujenzi wa Kituo cha Usahihishaji cha Mbezi Wani ambacho kinao uwezo wa kuweka washiriki  900 kwa wakati mmoja. 

Akizungumzia changamoto katika utekelezaji wa shughuli za Baraza la Mitihani, Dk. Msonde anaeleza baadhi ya changamoto kwamba  watu hutumia vyeti bandia katika kujipatia ajira, shule au vyuo.  

Anatoa mfano kwa kueleza kuwa katika mwaka wa fedha wa 2012/2013 jumla ya vyeti 1,891 sawa na asilimia 3.7 ya vyeti vyote 50,497 vilivyowasilishwa kwa ajili ya uhakiki vilibainika kuwa ni vya kughushi. Hata hivyo tatizo hilo limekuwa likipungua mwaka hadi mwaka baada ya NECTA kuanza kutoa vyeti venye picha.

Dk. Msonde anasema baraza linatoa wito kwa waajiri na Vyuo mbalimbali nchini kuhakikisha kuwa vyeti vinavyowasilishwa kwao vinaletwa Baraza la Mitihani kwa ajili ya kuhakikiwa. 

Anasema pia kuna udanganyifu ingawa vitendo vya udanganyifu katika mitihani vinazidi kupungua sana, kumekuwepo na vitendo vichache vya udanganyifu ambao hufanywa kwa mbinu mbalimbali kama vile kuingia na vijikaratasi vya kutazamia au kuandika majibu mwilini   na baadhi ya Wasimamizi kuwasaidia watahiniwa. 

Kwa mujibu wa baraza linaendelea kuimarisha usimamizi wa Mitihani na kuwachukulia hatua stahiki wale wote wanaobainika kujihusisha na udanganyifu katika mitihani.

Anasema baadhi ya shule na vyuo huwasajili wanafunzi wasio na sifa kinyume na taratibu za wizara, hivyo baraza linatoa wito kwa wakuu wa shule na vyuo vya ualimu kuhakikisha wanazingatia miongozo ya usajili inayotolewa na NECTA.

Related

UDAKU: AUNT EZEKIEL NA MARTIN KADINDA WABAMBWA WAKIFANYA YAO..WAHAHA KUJIELEZEA

MWANAMITINDO maarufu Bongo, Martin Kadinda na mwigizaji Aunt Ezekiel wamenaswa chobingo wakiwa katika pozi tata.Tukio hilo lililoibua maswali mengi yasiyokuwa na majibu lilitokea mwisho...

BURUDANI: ALI KIBA AFUNGUKA KUHUSU WANAO IDISI VIDEO YAKE YA "MWANA" HIKI HAPA ALICHOSEMA

Hatimaye Alikiba ameamua kuwajibu baadhi ya wapenzi wa muziki walioikosoa video ya wimbo wa ‘Mwana’ wanaodai kuwa haiendani na kile kinachoimbwa. Akizungumza na 255 ya XXL ndani ya Cloud...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item