jaridahuru

Mitandao

MICHEZO: SHIRIKISHO LA SOKA TANZANIA (TFF) LACHIMBA MKWARA MZITO, LAAHIDI KUTOFUMBIA MACHO VITENDO VYA RUSHWA



Dar es Salaam. Wakati pazia la usajili likifungwa leo, Bodi ya Ligi kwa kushirikiana na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limesisitiza kuwafungia wote watakaohusika na vitendo vya rushwa.
Mkurugenzi mpya wa mashindano, Boniface Wambura aliliambia gazeti hili kuwa TFF haitafumbia macho vitendo hivyo na kuwataka wachezaji na waamuzi kutojihusisha na vitendo hivyo.

“Kwa sasa awe kiongozi, mchezaji au mwamuzi atakayepatikana amejihusisha na vitendo vya rushwa au kupanga matokeo katika mchezo na ikabainika, tutamfungia maisha kujishughulisha na mpira.

“Hatutamwonea mtu lakini pia hatutampendelea mtu. Ndio maana kabla ya ligi tumekuwa tukijitahidi kutoa semina na kozi maalumu kwa waamuzi, ligi hii hatutakuwa na huruma na mtu,” alisisitiza Wambura.

Mechi mbalimbali za mpira wa miguu nchini, zinachezewa kwenye kamari kubwa kwa kununua mechi hizo kwa dau kubwa kabla ya mechi haijachezwa.

“Wachezaji na waamuzi waepuke kupanga matokeo ya mechi kwa ahadi za kupewa chochote kwenye mechi. Kufanya hivyo ni kudumaza soka nchini,” alisema. Hivi karibuni, rais wa TFF, Jamal Malinzi alisema kuwa zaidi ya waamuzi watatu wenye beji ya Fifa wamesimamishwa kuchezesha soka ndani na nje ya nchi kwa sababu ya kupanga matokea ya mechi. Alisema hadi sasa Fifa wanaendelea na uchunguzi wa tuhuma hizo na kuahidi adhabu kali kwa watakaobainika.

Related

Worldcup 2014 4743957682853940907

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item