jaridahuru

Mitandao

ELIMU: WANAFUNZI SHULE ZA MSINGI SASA KUSOMA KWA 'LAPTOP', WAZIRI MKUU ATHIBITISHA TAYARI KWA BAADHI YA SHULE

WAZIRI Mkuu, Bw. Mizengo Pinda, amesema Serikali itaendelea kutatua changamoto zinazokabili sekta ya elimu nchini kwa awamu ambapo hivi sasa, wanafunzi wa darasa la kwanza hadi la saba katika baadhi ya shule, wameanza kutumia kompyuta mpakato (laptop), zilizounganishwa na vitabu vyote wanavyopaswa kuvisoma wakiwa shuleni.

 

Bw. Pinda aliyasema hayo bungeni Mjini Dodoma jana katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo na kusisitiza kuwa, kompyuta hizo zitawasaidia wanafunzi kutobeba mzigo wa vitabu  

 

Majibu ya Bw. Pinda yalitokana na swali aliloulizwa na Mbunge wa Viti Maalumu, Bi. Mariam Msabaha (CHADEMA), aliyetaka kujua ni lini wanafunzi wa shule za Tanzania watatumia kompyuta mpakato darasani kama ilivyo kwa wanafunzi wa nchi jirani ya Kenya.

 

Akijibu swali hilo, Bw. Pinda alisema changamoto zinazoikabili sekta ya elimu ni nyingi hususan nyumba za walimu, madarasa ambapo kwa hivi sasa hitaji kubwa lipo zaidi kwenye shule za sekondari.

 

“Changamoto hizi zinaendelea kufanyiwa kazi...Serikali imechukua maamuzi makubwa juu ya suala hili lakini pia ni lazima Bajeti ya Wizara ya Elimu izidi kukua ili tuendelee kuzifanyia kazi,” alisema Bw. Pinda.

 

Upinzani wakubali hoja

Katika hatua nyingine, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, jana imeunga mkono hoja iliyotolewa bungeni na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Bi. Jenista Mhagama kuhusu Chuo cha Ustawi wa Jamii Tengeru kuwa taasisi inayojitegemea.

 

Kwa nyakati tofauti, baadhi ya wabunge wa upinzani waliunga mkono hoja hiyo na kuitaka Serikali iangalie jinsi ya kuzitatua changamoto zilizopo katika chuo hicho likiwemo tatizo la ardhi na kujenga maktaba.

 

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Bw. Stephen Wassira, alisema inafurahisha kuona upinzani wananga mkono hoja hiyo lakini wasiiachie Serikali pekee kutatua changamoto zilizopo.

 

Alisema jambo la msingi ni jinsi gani wahitimu wa chuo hicho wataweza kutumika kwenye jamii ili kuleta maendeleo nchini ambapo kuwatumia watu hao ni kitu cha msingi.

 

Mbunge wa Viti Maalumu, Bi. Cecilia Pareso (CHADEMA), naye aliunga mkono hoja ya chuo hicho kujitegemea ili kiweze kutoa wataalamu wa maendeleo ya jamii ambao wengi wao ndio wanaosimamia miradi mingi ya Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF).

 

“Mimi ni mjumbe katika kamati hiyo iliyokwenda kuangalia mazingira ya chuo hiki...baada ya ombi hili kukubalika tunataka bodi iundwe haraka kwani kumekuwa na ucheleweshaji wa kuundwa kwa bodi katika maeneo mengi.

 

“Pia tatizo la ardhi katika chuo hiki, lipatiwe ufumbuzipamoja na kuweka miundombinu...sh. bilioni moja zinahitajika ili kujenga maktaba ya kisasa,” alisema Pareso.

 

Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa (CHADEMA), alisema kwa mara ya kwanza anaunga mkono hoja bila tatizo ambapo vyuo kama hivyo vinapaswa kutumika kwa kubadili fikra tofauti.

 

Wabunge wengine waliuunga mkono hoja hiyo ni Bw. Moses Machali na Bw. Kombo Khamis Kombo ambao licha ya kuunga mkono hoja, walitaka kujua ni jinsi gani Serikali itahakikisha chuo hicho kitapata fedha za kutosha ili kiweze kujiendesha chenyewe.

Related

JH STORY: NILIVYO AMBUKIZWA UKIMWI (DAR)

TABATA October 06, 2009 Siku ya Jumanne. Background: Nilikuwa nimemaliza zangu chuo MUCCoBS kozi ya BAF na kufanikiwa kupata GPA nzuri tu ya 4.2. Nilikuwa na matumaini na ndoto nyingi za mbe...

SIASA: UKAWA WASHAURIWA KURUDI KUJADILI KATIBA YA WATANZANIA NA KIONGOZI WA UNDP

KIONGOZI wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP), Helen Clark, ameshauri wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, waliojiundia kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), kurejea kujadili ...

KIMATAIFA: WATU 157 WAFA KATIKA MGODI WA MAKAA YA MAWE UTURUKI

Mlipuko katika mgodi wa makaa ya mawe magharibi mwa Uturuki umesababisha vifo vya zaidi ya wachimbaji migodi 150 na kujeruhi wengine zaidi ya 70 kwa mujibu wa maafisa nchini humo. ...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item