jaridahuru

Mitandao

BUNGENI: JINSI KATIBA ILIVYO WAGAWA WANANCHI WA TANZANIA


Dar es Salaam. Mbali na kubaki ‘njia panda’ , kuna baadhi ya Watanzania ambao wanaamini mshale wa saa bado unaendelea kuonyesha dalili na matumaini ya kupatikana kwa Katiba Mpya.
Hatua hiyo inatokana na safari ndefu ya takriban miezi 26 tangu Mchakato wa Katiba uanze Aprili 6, 2012, huku hatua mbalimbali zikipitiwa, ikiwamo ukusanyaji wa maoni ya wananchi.
Hata hivyo, hatua iliyobaki inasubiria sala na jicho la imani kutokana na upande wa kundi moja la Wajumbe wa Bunge la Katiba (Ukawa), kutofahamika kwamba utarejee bungeni au la.
Hiyo imetokana na mvutano uliojitokeza wakati wa mjadala wa sura mbili tu za awali, zinazopendekeza Muundo wa Muungano wa Serikali tatu.
Mpasuko huo wa Wajumbe wa Bunge la Katiba, umeenda mbali zaidi na kuwagawa Watanzania ambao nao wako njia panda kuhusu uwezekano wa kupatikana kwa katiba hiyo mpya wanayoitazamia.
Makundi yanayoonekana kuwa njia panda ni yale ya wanaharakati, vyombo vya habari, wanasiasa nguli na wasomi wanaotegemewa. Wanasiasa ndiyo waliofanikiwa kuuteka mchakato huu.
Vyombo vya habari
Kwa mujibu wa takwimu za Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Tanzania kuna vituo 93 vya redio, 28 vya televisheni na magazeti 537 yenye mitazamo, sera, itikadi tofauti.
Katika mchakato huo, vyombo vya habari vilianza kuripoti katika mitazamo mbalimbali inayolenga kuelimisha, kukosoa juu ya kila hatua inayojitokeza. Hata hivyo, mjadala huo wa Katiba ulipofikia sasa umewezesha kujenga mpasuko mkubwa miongoni mwa wanahabari kama ilivyo kwa wanasiasa na makundi mengine.
Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF), Ernest Sungura anasema inasikitisha kuona mwandishi wa habari anapoyumbishwa na itikadi za kisiasa.
Sungura ambaye pia ni mwandishi nguli anaongeza kuwa taaluma ya habari ina msingi pekee wa kusimamia, kueleza watu ukweli katika jambo lolote linalojitokeza kwenye jamii.
“Tulitegemea kuona nafasi hii ya mjadala wa Katiba waandishi ndiyo wajikite kuchambua, kutueleza ukweli, lakini wameingia kwenye mitego ya wanasiasa,” anasema na kuongeza:

“Mwandishi unaweza kuandika kama maoni yako kupitia kolamu, yawe ni mawazo yanayoeleza ukweli pia lakini inapofikia hatua ya kuandika hoja za muundo wa serikali lazima kuhakikisha unaandika bila upendeleo na kwa usawa.”
Aidha, anabainisha kwamba, waandishi kuajiriwa katika vyombo vyenye itikadi, sera na mitazamo tofauti ni moja kati ya sababu kuu iliyosababisha kuyumbishwa kitaaluma.
Wasomi
Wasomi nao wamekuwa wakitazamwa kwa jicho la kuleta mapinduzi kwa jamii ya Watanzania. Lakini nao wamejikuta wakisambaratishwa na kujikuta wakigawanyika makundi mawili. Wanaopingana na rasimu iliyopendekeza Serikali tatu na wanaoiunga mkono rasimu hiyo ya tume.
Pamoja na elimu yao, masilahi ya wanasiasa yamepenyeza kwa wanasheria ambao wamekuwa wakiendea kutofautiana kimtazamo juu ya uhalali wa kisheria katika Mkataba wa Muungano .
Mchakato huo wa Katiba pia umewasambaratisha wachumi kupitia kipengele hicho cha Muundo wa Serikali. Wenyewe wanagawanyika wakishindanisha hoja zao kuhusu gharama za uendeshaji wa serikali hizo.
Viongozi wa dini
Katika hatua ya kushangaza zaidi hata viongozi wa imani mbalimbali za dini wamejikuta kwenye mpasuko wa makundi mawili.
Viongozi hao wa dini kutoka madhehebu ya Kikristo na Kiislamu wameonyesha mitazamo tofauti katika kutafuta ukweli juu ya muundo gani wa serikali ambao unafaa kwa Watanzania ndani ya Katiba ijayo.
Kuna baadhi ambao wanaonyesha msimamo wao juu ya maoni ya rasmu ya Katiba, huku wengine wakiunga mkono hoja za upande wa serikali mbili, zinazopigiwa chapuo na CCM.
Wanaharakati
Kundi la wanaharakati ni miongoni mwa Watanzania waliojizolea umaarufu na imani kubwa kwa wananchi. Katika kundi hilo pia kuna wasomi, viongozi wa mashirika, asasi na taasisi za kijamii.

Hata hivyo, kwa bahati mbaya zaidi nao wamegawanyika.Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bashiru Ally anasema inasikitisha kuona fikra za wanaharakati zinageuzwa na masilahi ya wanasiasa.
Anasema kundi hilo limefika pabaya kutokana na kujihalalishia kibali cha kutafuta ukweli kuhusu Mchakato wa Katiba, huku wakiwa wamefunikwa na mkono wa masilahi ya wanasiasa.
“Mimi nimekuwa nikiogopa hata kuzungumza kutokana na mazingira hayo, lakini kuna tofauti kubwa kati ya kutofautiana mitazamo na mpasuko, kinachoonekana kwa sasa ni mpasuko unaotokana na upotoshwaji kabisa,” anasema Bashiru na kuongeza:
“Watanzania hawawezi kujadiliwa hoja zao. Kilichobakia wanaharakati wanatumikishwa kwa rushwa na makundi hayo ya wanasiasa, tungewaachia wananchi wenyewe, wala tusiingilie na kupotosha ukweli. .

Related

DIWANI KITETO ACHOMWA MKUKI NA WAFUGAJI

Kiteto. Diwani wa Kata ya Kaloleni eilayani Kiteto mkoani Manyara, Christopher Parmet amenusurika kufa baada ya kuchomwa mkuki na wafugaji wa eneo hilo wakati akifukuza mifugo iliyovamia shamba lake...

IFAHAMU MITAA HATARI ZAIDI KWA UPORAJI MJINI DAR, COCOA BEACH YATAJWA

Kufuatia tukio lililowasikitisha na kuwashangaza wengi katika miji ya dar na sehemu zingine za Tanzania la kuporwa na kutobolewa macho kwa kijana mmoja maeneo ya buguruni, gazeti la Nipashe la tar...

RAIS MAGUFULI AMTEUA HUYU KUWA MKURUGENZI MTENDAJI WA TCRA

Rais wa Jamhuru ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli amemteua Eng. James Mitayakingi Kilaba kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, TCRA.

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item