jaridahuru

Mitandao

MAKALA / JAMII: FAHAMU JINSI FREEMASON ILIVYOINGIA TANZANIA, WAJUE VIONGOZI WAKWANZA NA MFUMO WA KIUTENDAJI



Wiki iliyopita, mwandishi wa simulizi hizi, Kiongozi Mstaafu wa Freemason Afrika Mashariki, Sir Andy Chande, alieleza namna Dikteta Idi Amin alivyowatimua Freemason Uganda.

Hatua iliyosababisha jengo lililokuwa linatumika kugeuzwa kuwa kanisa.
Pia alieleza nanma watu wenye asili ya Afrika Mashariki walivyochangamkia kujiunga na Freemason, kiasi cha kuanzisha ofisi za watu weusi peke yao. Endelea...

Mwaka 1977 tulishuhudia Visiwa vya Ushelisheli vikijiunga na Ofisi kuu ya Freemason Afrika Mashariki. Baada ya kusubiri kwa muda mrefu, mwaka huo huo Septemba ilifunguliwa ofisi ya Freemason ya Ushelisheli iliyopewa namba 8798 huko Victoria, mahe.

Mizizi ya Freemason katika Visiwa vya Ushelisheli ilianza kukua mwanzoni wakati wa ujio wa mafundi kutoka Uingereza. Leo Freemason imeendelea kupata nguvu na heshima katika kila kona ya visiwa hivyo.

Hivi sasa wanachama wa Freemason katika visiwa hivyo wanaendelea kufanya kazi vizuri katika wilaya zote.

Ofisi ya kumi ya Freemason na isiyo na wanachama wazungu ilifunguliwa Tanzania chini ya Mkuu wa Afrika Mashariki, jambo lilitajwa kuwa ni la heshima, hasa ikikumbukwa historia ya Freemason Afrika Mashariki.

Baadaye nilikuwa nikiitwa sehemu mbalimbali Afrika Mashariki kwa ajili ya kuzindua ofisi mpya za Freemason, wakati huo mbinu mpya zilikuwa zimeanza kutumika kuboresha huduma zetu.
Ofisi ya kwanza ya mwongozo ya Freemason ilifunguliwa Nairobi nchini Kenya, chini ya Mkuu wa Ofisi hizo wa Afrika Mashariki na kusimamiwa na ofisi ya Harmon namba 3084, iliyotumika kama makao makuu kwa ofisi zote za Nairobi.

Baada ya kufunguliwa ofisi hiyo, haraka haraka ikafunguliwa ofisi nyingine huko Kampala nchini Uganda. Ofisi hiyo ilikuja kutumika kwa ajili ya eneo la bara la Afrika Mashariki.

Maendeleo hayo mapya yalikuja kuwa kichocheo kikubwa cha maendeleo katika nyanja mbalimbali ikiwamo elimu. Mafanikio hayo yalitajwa dhahiri kwenye mikutano ya mwaka ya Freemason Afrika Mashariki ambayo imekuwa ikifanywa kila mwaka tangu mwaka 1989.

Hatua hiyo iliongezwa nguvu na baadhi ya viongozi wasomi na wenye uelewa wa kutosha waliotoa mapendekezo mbalimbali ya kuiimarisha Freemason. Hayo yote yalisaidia kuongezeka kwa mawazo mazuri namna ya kuendesha Freemason.


Mwaka 1990 Afrika Mashariki ilishuhudia ujio wa wageni wakubwa wawili; kiongozi mstaafu Lord Cornwallis na James Stubbs, waliowahi kuwa viongozi wa juu wa Freemason.
Viongozi hao waliitembelea Tanzania na nchi nyingine za Afrika Mashariki huku wakitoa mchango mkubwa uliosaidia kuinua zaidi Freemason.

Wakiwa Dar es Salaam, Lord Cornwallis alikwenda kuvua samaki katika Bahari ya Hindi na kurudi na aina ya samaki ambayo haikuwahi kuonekana kwa zaidi ya miaka 50, jambo lililofanya samaki hao kuitwa ‘samaki wa Cornwallis’.

Pia miaka ya 1990 ilitokea changamoto nyingine iliyodumu kwa muda mfupi dhidi ya Freemason Afrika Mashariki, ikilenga ofisi ya Kenya. Aliyekuwa Rais wa Kenya wakati huo, Daniel arap Moi aliunda tume ya kuchunguza watu wanaoabudu shetani, ambapo moja ya majukumu ya tume yalikuwa ni kuichunguza Freemason.

Nilifika mbele ya tume hiyo mara mbili katika nyakati tofauti kama Mkuu wa Freemason Afrika Mashariki. Nilitoa ushahidi kuhusiana na kazi tunazozifanya.

Nilipokwenda mara ya pili kukutana na tume hiyo, tulitembelea ofisi ya Ukumbi wa Freemason wa Nairobi, huku tukiwa na wapiga picha waliopiga picha nyingi sana.
Japokuwa tume haikutoa majibu ya kazi waliyoifanya, tulipata taarifa kuwa walikuwa wametusafisha na tuhuma zilizokuwa zinaikabili Freemason.

Nafurahi kusema kuwa tuhuma zile zilisafishwa zaidi na Rais aliyefuata baadaye, Mwai Kibaki, ambaye katika moja ya hotuba zake alisema kuwa Freemason imetoa mchango mkubwa sana Kenya.
Tangu wakati huo, aliyewahi kuwa Makamu wa Rais wa Kenya wakati fulani, Moody Awori, alikuwa akiutembelea ukumbi wa Freemason wa Nairobi na kunywa chai na baadhi ya wanachama. Pia alikuwa akipokea michango mbalimbali iliyotolewa kwa vikundi na taasisi.

Toa Comment ili tuendelee

Related

Jamii 8379283687986738241

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item