jaridahuru

Mitandao

SIASA: KIU YA URAIS 2015 YAMPONZA PINDA, JUKWAA LA KATIBA LADAI IMEZOROTESHA UTENDAJI SERIKALINI

Waziri wa Mizengo Pinda ametangaza nia ya kutaka urais mwaka 2015.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda ametangaza nia ya kutaka urais mwaka 2015.

Kufuatia Waziri mkuu wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda kutangaza kuwania Urais mwakani hatimaye jukwaa la katiba limetoa kauli kuhusiana na maamuzi hayo ya waziri mkuu wa nchi. Nia hiyo aliitoa Wiki iliyopita Ikulu ndogo ya Mwanza , mara baada ya kuwaalika wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) toka mikoa sita ya Kanda ya Ziwa

Pinda aliyekuwapo jijini Mwanza kwa ajili ya kuendesha harambee ya Mfuko wa Taasisi ya Benjamin Mkapa iliyofanyika wiki iliyopita, alikutana kwa ‘mafungu’ na wajumbe zaidi ya 50 kutoka Mara, baadhi toka Mwanza, Geita na Kagera.

Aidha, Jukwaa la Katiba nchini limeibuka na kusema kuwa kitendo alichokifanya Waziri huyo mkuuu kimezorotesha utendaji serikalini, hii ni kutokana na kauli hiyo kuchochea uhasama kwa watumishi wa Umma.

Kwa mujibu wa Kaimu Mwenyekiti wa jukwaa la Katiba nchini Hebron Mwakagenda ambapo amesema Waziri mkuu huyo alikosea kuzungumza nia yake mapema huku akijua bado ni msimamizi wa Shughuli za serikali. Kaimu mwenyekiti amesema hayo katika mkutano na waandishi wa Habari leo jijini Dares salaam.

Amesisitiza kuwa Taifa litegemee kusinyaa kwa utendaji serikalini kutokana Nia hiyo aliyotangaza Waziri mkuu kwani sasa wakuu wa Wilaya na Mikoa wameanza kujigawa kimakundi na kila mtu kuanza kipigia debe upande wake anaoutaka na kuleta misuguano ndani ya Serikali.

Related

Siasa 8801388962715371491

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item