jaridahuru

Mitandao

CURLING: VAN GAAL WA MAN U ADAI ALITEGEMEA KIPIGO WALICHOPATA CHA 4:0 USIKU WA JUMANNE

Mshambuliaji Javier Hernandez Chicharito kulia wa Man United akigombea mpira na beki wa MK Dons
Mshambuliaji Javier Hernandez Chicharito kulia wa Man United akigombea mpira na beki wa MK Dons

Kocha wa Manchester United, Louis van Gaal amesisitiza kuwa “hakushtushwa kamwe” kwa kikosi chake kukubali kipigo cha mabao 4-0 kutoka kwa Milton Keynes (MK) Dons, katika mechi ya Kombe la Capital One juzi usiku.

Man United ilitupwa nje ya michuano hiyo na kikosi cha Dons kinachoshiriki League One, na kumuacha Van Gaal akiwaongoza Mashetani Wekundu hao wa Old Trafford bila kuambulia ushindi katika mechi tatu mfululizo za kimashindano tangu alipoanza kaazi.

“Mimi binafsi sikushtushwa na kipigo hiki, kwa sababu nilijua nini kitatokea,” alisema Van Gaal na kuongeza: “Timu mpya kamwe haiwezi kujengwa kwa mwezi mmoja.

“Lakini pia nadhani Milton Keynes walicheza vizuri sana, walikuwa makini na mwisho wa yote walikuwa na bahati ya kupata mabao,” alisema Van Gaal kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Uholanzi aliyechukua mikoba ya David Moyes.

Kosa lililofanywa na beki Jonny Evans lilimzawadia Will Grigg bao la uongozi na mshambuliaji huyo wa MK Dons alifunga la pili baada ya saa moja tangu bao hilo. Mshambuliaji wa Arsenal anayecheza Dons kwa mkopo, Benik Afobe alifunga mabao mawili katika mechi ambayo Man United ilipiga mashuti mawili tu langoni kwa wapinzani.

Van Gaal alienda mbali kwa kusema aliamua kupanga kikosi tofauti katika jaribio la kukiangalia kikosi cha pili cha timu yake baada ya sare ya mwishoni mwa wiki iliyopita ya bao 1-1 dhidi ya Sunderland na kukiri namna kikosi chake kilivyokithirisha makosa.

“Tulifanya makosa mengi mno mchezoni. Mimi sijutii uteuzi wangu wa kikosi, lakini mabadiliko yalikuwa hatari kwetu.

“Nililazimika kubadili mfumo tuliochezea katika kipindi cha kwanza. Tulicheza mmoja dhidi ya mmoja kwa kikosi kizima uwanjani na nadhani uliliona hilo. Tulitengeneza nafasi nyingi, lakini kamwe hatukuwa na bahati,” alisema Van Gaal.

Van Gaal alichukua mikoba ya kufanya kazi Old Trafford kiangazi hiki, akibeba hatamu za Moyes, aliyeiongoza timu kumaliza Ligi Kuu ikiwa nafasi ya saba, katika msimu ulioweka rekodi ya matokeo mabaya zadi kwao kwenye historia ya Ligi Kuu.

Man United ikamtimua kazi Moyes mechi chache kabla ya kumaliza msimu, na ujio wa Van Gaal ukaenda sambamba na matumizi makubwa ya fedha katika usajili, ambako tayari imetumia kitita cha pauni mil. 131.7, zikiwamo pauni mil. 59.7 ilizotumia Jumanne kumnasa winga Angel Di Maria kutoka Real Madrid.

Related

Sports 8941984989858210621

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item