jaridahuru

Mitandao

SIASA: ONYO LA CHADEMA KWA WAGOMBEA WAKE LAMTIA KIWEWE FREEMAN MBOWE, ATAKA APELEKEWE FOMU



CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema wagombea wa nafasi za kitaifa hawaruhusiwi kukutana na wajumbe wapiga kura waliyoko mikoani, kwani kwa kufanya hivyo kuna mianya ya rushwa na atakayebainika ataondolewa kwenye kinyang’anyiro.

Chama hicho, pia kimesisitiza kuwa suala la kugombea ni hiari ya kila mwanachama wala sio suala la uongozi wa ngazi yoyote ya chama, hivyo kila mgombea atekeleze wajibu kwa kujaza fomu, kuzilipia na kuzifikisha ofisini kwa utaratibu uliowekwa.

Hayo yamebainishwa jijini Dar es Salaam jana na Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Uratibu wa Kanda wa CHADEMA, Benson Kigaila, wakati akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam.

Kigaila, alitoa msisitizo huo kukazia kanuni za kampeni na rushwa za chama hicho, huku akitoa taarifa kuwa zoezi la kuchukua fomu na kurejesha kwa nafasi za kitaifa limeongezewa hadi Agosti 30 mwaka huu badala ya Agosti 25 iliyokuwa imetangazwa awali.

“CHADEMA kuna kanuni za Uchaguzi na kanuni kuhusu namna ya kudhibiti vitendo vya rushwa, na kwa mujibu wa kanuni hizo, wagombea hufanya kampeni ukumbini siku ya Uchaguzi,” alisema.

Akieleza sababu za kuongeza muda huo, Kigaila alisema kuwa bado kuna chaguzi mbalimbali zinafanyika ngazi za mikoa, hivyo sekretarieti ya chama hicho iliyokutana Dar es Salaam juzi, iliamua kuongeza ili wagombea wengine watakaoshinda kwenye ngazi za mikoa, wapate pia fursa ya kugombea nafasi mbalimbali za kitaifa.

Kuhusu taarifa za uchaguzi, alisema umekamilika ngazi za misingi, mitaa, shehia kwa upande wa Zanzibar na matawi. Ngazi za kata majimbo na wilaya, pia zimekamilika na hadi jana ilitarajiwa mikoa 25 itakuwa imekamilisha na kubakiza saba tu itakayohitimisha kabla ya Agosti 30.

Katika hatua nyingine, zoezi la kumkabidhi Mwenyekiti wa Taifa wa Chama hicho fomu yake na kumshawishi agombee, halikufanyika kama ilivyotarajiwa jana.

Mmoja wa watoa taarifa ambaye aliomba asitajwe gazetini, alisema baada ya zoezi hilo kuungwa mkono na wazee wa Dar es Salaam na Pwani, taarifa imepelekwa kwa Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe, na sasa anatafuta wakati muafaka wa kukutana na wazee hao waliyotoka Kigoma kumletea fomu aweze kutetea kiti hicho.

Aidha, kuhusu tarehe ya uchaguzi mkuu, Kigaila alisema CHADEMA haitabadilisha na itabaki Septemba 14 kwenye ukumbi wa Mlimani City.

Taarifa za uhakika kutoka ndani ya CHADEMA, zinasema mkutano wa ufunguzi wa uchaguzi huo utarushwa moja kwa moja na kituo cha runinga kwa saa tatu na pia wakati wa kutangaza matokeo, pia matangazo yatarushwa moja kwa moja.

Related

Siasa 8328661215860468459

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item