jaridahuru

Mitandao

SIASA: ONYO LA CHADEMA KWA WAGOMBEA WAKE LAMTIA KIWEWE FREEMAN MBOWE, ATAKA APELEKEWE FOMU



CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema wagombea wa nafasi za kitaifa hawaruhusiwi kukutana na wajumbe wapiga kura waliyoko mikoani, kwani kwa kufanya hivyo kuna mianya ya rushwa na atakayebainika ataondolewa kwenye kinyang’anyiro.

Chama hicho, pia kimesisitiza kuwa suala la kugombea ni hiari ya kila mwanachama wala sio suala la uongozi wa ngazi yoyote ya chama, hivyo kila mgombea atekeleze wajibu kwa kujaza fomu, kuzilipia na kuzifikisha ofisini kwa utaratibu uliowekwa.

Hayo yamebainishwa jijini Dar es Salaam jana na Mkurugenzi wa Oganaizesheni na Uratibu wa Kanda wa CHADEMA, Benson Kigaila, wakati akizungumza na waandishi wa habari makao makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam.

Kigaila, alitoa msisitizo huo kukazia kanuni za kampeni na rushwa za chama hicho, huku akitoa taarifa kuwa zoezi la kuchukua fomu na kurejesha kwa nafasi za kitaifa limeongezewa hadi Agosti 30 mwaka huu badala ya Agosti 25 iliyokuwa imetangazwa awali.

“CHADEMA kuna kanuni za Uchaguzi na kanuni kuhusu namna ya kudhibiti vitendo vya rushwa, na kwa mujibu wa kanuni hizo, wagombea hufanya kampeni ukumbini siku ya Uchaguzi,” alisema.

Akieleza sababu za kuongeza muda huo, Kigaila alisema kuwa bado kuna chaguzi mbalimbali zinafanyika ngazi za mikoa, hivyo sekretarieti ya chama hicho iliyokutana Dar es Salaam juzi, iliamua kuongeza ili wagombea wengine watakaoshinda kwenye ngazi za mikoa, wapate pia fursa ya kugombea nafasi mbalimbali za kitaifa.

Kuhusu taarifa za uchaguzi, alisema umekamilika ngazi za misingi, mitaa, shehia kwa upande wa Zanzibar na matawi. Ngazi za kata majimbo na wilaya, pia zimekamilika na hadi jana ilitarajiwa mikoa 25 itakuwa imekamilisha na kubakiza saba tu itakayohitimisha kabla ya Agosti 30.

Katika hatua nyingine, zoezi la kumkabidhi Mwenyekiti wa Taifa wa Chama hicho fomu yake na kumshawishi agombee, halikufanyika kama ilivyotarajiwa jana.

Mmoja wa watoa taarifa ambaye aliomba asitajwe gazetini, alisema baada ya zoezi hilo kuungwa mkono na wazee wa Dar es Salaam na Pwani, taarifa imepelekwa kwa Mwenyekiti wa Chama hicho Freeman Mbowe, na sasa anatafuta wakati muafaka wa kukutana na wazee hao waliyotoka Kigoma kumletea fomu aweze kutetea kiti hicho.

Aidha, kuhusu tarehe ya uchaguzi mkuu, Kigaila alisema CHADEMA haitabadilisha na itabaki Septemba 14 kwenye ukumbi wa Mlimani City.

Taarifa za uhakika kutoka ndani ya CHADEMA, zinasema mkutano wa ufunguzi wa uchaguzi huo utarushwa moja kwa moja na kituo cha runinga kwa saa tatu na pia wakati wa kutangaza matokeo, pia matangazo yatarushwa moja kwa moja.

Related

SIASA: ZITTO AIBUA UOZO MWINGINE WA MAPATO YA TANZANITE, WAZIRI MGENI WA NISHATI AKIONA KITI KICHUNGU

Dodoma. Bunge limeagiza kuwa swali lililoulizwa na Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Kidawa Hamid Saleh kuhusu kiasi cha mapato yaliyotokana na mauzo ya Tanzanite katika kipindi cha mwaka 2011 ha...

BUNGENI: YULE MBUNGE WA CCM ALIYEISHAURI SERIKALI KUWAFUNGA KIZAZI WANAUME ILI KUPUNGUZA IDADI YA WATU..ATOA MPYA!

Wabunge wametaka kuwepo na udhibiti wa ongezeko la watu nchini kwa  kutaka wanaume wadhitibiwe katika uzazi, kama ilivyo kwa wanawake huku wengine wakitaka serikali kuboresha rasilimali bila k...

SIASA: MIAKA 38 YA CHAMA CHA MAPINDUZI, WENGI WAHOJI FALSAFAYA RASI BORA LAZIMA ATOKE CCM NI YA KWELI?

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) mwishoni mwa wiki iliyopita kimeadhimisha miaka 38 tangu kuzaliwa kwake katika kaya hii. Mazuri na mabaya yake sitayajadili leo bali nitaangalia jambo moja nalo n...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item