jaridahuru

Mitandao

EBOLA: KIGOMA YAANZA KUCHUKUA TAHADHARI ZA KUJIKINGA NA UGONJWA WA EBOLA KUFUATIA KUINGIA KWA EBOLA CONGO

Ugonjwa wa ebola umeingia nchini Congo DRC.Tanzania yajihadhari.
Ugonjwa wa ebola umeingia nchini Congo DRC.Tanzania yajihadhari.

Kufutia kuenea taarifa ya kuwepo wagonjwa nane wenye ugonjwa wa ebola nchini Congo DRC, Mkoa wa kigoma umeamua kuchuakua hatua kukabiliana na maingiliano ya watu mkoani humo.

Aidha, kutoakana na ujirani wa mkoa wa Kigoma na Congo DRC mkuu wa mkoa wa Kigoma Ndugu Issa Machibya amesema kwamba mkoa huo umeanza kuchukua tahadhari kwenye mipaka wa Tanzania na Congo DRC.

Ameongeza kwamba “ nimemuagiza katibu tawala wa mkoa magari yote yenye uwezo wa kubeba vipaza sauti usiku au jioni watu wamesharudi nyumbani yapite kutangazia Wananchi kwa muda wa siku tatu mfululizo licha ya kuweka vipeperushi kuhusu dalili na jinsi ya kujikinga na ugonjwa wa ebola”

Kwa upande wa John Ndunguru katibu tawala wa mkoa amesema hospitali za mkoa huo zimeshatenga chumba maalumu ili kama mgonjwa akitokea awekewe kinga au wigo kwa muda wa siku 48.

Related

Jamii 5073898551846776114

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item