jaridahuru

Mitandao

TZ: MOROCCO YAITOLEA NJE TAIFA STARS MECHI ILIYOOMBA YA KIRAFIKI, SASA TAIFA STARS YAWAMEZEA MATE WARUNDI

Wachezaji wa timu ya Taifa ya soka ya Tanzania wakiwa mazoeini.
Wachezaji wa timu ya Taifa ya soka ya Tanzania wakiwa mazoeini.

Baada ya kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania Mart Nooij kutangaza kikosi kitakacho cheza na timu ya Taifa ya Morocco mchezo wa kirafiki hapo Septemba 5, waarabu hao wamefuta ombi lao la kujipima na Tanzania kama walivyo oba awali.

Morocco ndio iliomba kucheza na Tanzania katika tarehe hiyo lakini  wametuma ujumbe katika shirikisho la soka Tanzania kuwa hawata weza kucheza mchezo huo.

Akizungumza na mwandishi wetu Katibu mkuu wa TFF Selestine Mwesigwa amesema kuwa Morocco wameghairi kucheza wakidai kuwa asilimia kubwa ya wachezaji wa timu hiyo wako kwenye michuano mbali mbali kwenye klabu zao na hivyo hawata weza kuacha na kuja kucheza mchezo wa kirafiki.

Baada ya Wamorocco hao kujiondoa huku kikosi cha Taifa Stars kikitarajia kuingia kambini Agosti 31, Kocha mkuu Nooij ameamua kuichagua Burundi ili waweze kujipima katika tarehe hiyo.

Kwa mara ya mwisha Tanzania na Burundi zilipokutana Stars ililala chini kwa kichapo cha bao 3-0 mbele ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dk. Jakaya M. Kikwete katika sherehe za muungano.

Related

Sports 6520085108395846654

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item