jaridahuru

Mitandao

KIMATAIFA: BOKO HARAM YAZIDI KUUA NIGERIA, WATU WENGINE 25 WAUAWA KATIKA BOMU

Wanamgambo wa kiislamu, Boko Haram wamekuwa wakitekeleza mashambulizi kadha wa kadha ya mabomu na mauaji nchini Nigeria tangu walipoanza Operesheni yao mwaka 2009 wakiwa na nia ya kuunda nchi ya kiislamu. Boko Haram huwashambulia viongozi wa kiislamu ambao hukosoa misimamo yao.
 


Jeshi la polisi nchini Nigeria limetoa taarifa ya kuuawa takriban watu 25 kutokana na mlipuko wa bomu ulio tokea leo jioni katika barabara ya Isa Kaita mjini Kaduna.Bomu hilo lilimlenga Kiongozi wa dini ya kiislamu mwenye msimamo wa wastani Dahiru Bauchi ambaye alikua akitoka kuhubiri katika viwanja vya Murtala Muhammed. Bauchi amenusurika katika shambulio hilo, hajajeruhiwa halikadhalika bado haijajulikana waliofanya shambulio hilo.

 

 

 

Related

Kimataifa 2374428198801135004

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item