jaridahuru

Mitandao

SIASA: VIONGOZI WAPYA CHADEMA KURINDIMA AGOSTI 3 UBUNGO DAR ES SALAAM KWA MYIKA

UONGOZI mpya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo wilaya ya kichama Ubungo unatarajiwa kujulikana Agosti 3 mwaka huu baada ya uchaguzi wa ngazi za chini katika wilaya hiyo kukamilika.
Mbali na viongozi wa wilaya hiyo kujulikana siku hiyo, pia chama hicho kimeeleza kuwa, kimejiandaa vema kuwadhibiti mamluki wasijipenyeze katika uongozi huo.

Hayo yalibainishwa na Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Ubungo, Goodluck Justine, wakati akielezea mafanikio yaliyopatikana katika uchaguzi wa ngazi za msingi, matawi na kata.

Justine alisema, ni fursa kwa kila mwanachama muadilifu wa CHADEMA Wilaya ya CHADEMA Ubungo kuwania nafasi anayoona ataimudu.

Aliongeza kuwa, katika uchaguzi wa ngazi za chini, chama hicho kimefanikiwa kujiimarisha na kuongeza wanachama zaidi.

Alisema, fomu zimeanza kutolewa jana na mwisho wa kuchukua na kurejesha itakuwa Agosti Mosi saa 10 jioni

Related

Siasa 2619490876354093732

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item