jaridahuru

Mitandao

SIASA: MKOSAMALI AFUNUA UKWELI WA KUTISHA KUHUSU PHIILIP MANGULLA KATIKA ZIARA YA MUHAMBWE, HUU NI WIZI


MBUNGE wa Muhambwe mkoani hapa, Felix Mkosamali (NCCR Mageuzi), amemlipua Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Philip Mangula akidai kuwa ameondoka katika hoteli aliyofikia bila kulipa pango.

Akihutubia mamia ya wananchi wa Kibondo mkoani hapa jana kwenye mkutano wa hadhara, Mkosamali alisema Mangula alifanya hivyo alipokuwa katika ziara ya mikutano ya ndani ya chama hicho katika Jimbo la Muhambwe.

Mkosamali aliyasema hayo katika mfululizo wa mikutano ya NCCR-Mageuzi mkoani Kigoma, ikiongozwa na Katibu Mkuu wa chama hicho, Mosena Nyambambe, Naibu Katibu Mkuu, Moses Machali ambaye pia ni Mbunge wa Kasulu Mjini na Katibu Mwenezi, David Kafulila ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kusini.

Mbunge huyo alisema awali, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa alitaka kufikia hotelini hapo, lakini Mkuu wa Wilaya ya Kibondo, Venance Mwamoto aliuambia uongozi wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) linalomiliki hoteli hiyo kuwa Dk. Slaa haruhusiwi kufikia hapo.

“Nimeshindwa kuelewa, ilikuwaje Dk. Slaa akazuiliwa kufikia katika hoteli hiyo, lakini Mangula amefikia katika hoteli hiyo, tena akaishi na kuondoka bila kulipia? Tunajifunza nini? Kwanini CCM wanaendelea kutumia madaraka yao vibaya?” alihoji Mkosamali.

Aidha, Mkosamali aliwaambiwa wananchi wa Kibondo kuwa anakerwa na tabia ya DC Mwamoto, kwani amekuwa akiwaelekeza askari wa Jeshi la Wananchi kuwapiga raia hata wanaokwenda hospitalini, kwa kile kilichoitwa kufanya usafi wa mji wa Kibondo siku ya Alhamisi.

“Usafi tunapenda wote, lakini DC amekuwa akiwatumia JWTZ kuwapiga wananchi wasiofika kufanya usafi hata kama wanakwenda hospitali, raia wanapigwa wanalazwa.

“Sasa ni utekelezaji gani huu wa sheria hata kama usafi tunapenda? Tena siku hizi ukikamatwa unakula muwa unalipishwa 5,000 kwa amri ya mkuu wa wilaya, mbona mambo haya hatukukubaliana katika vikao? Kwanini DC anaruhusu ufisadi wa aina hii?” alihoji Mkosamali.

Katika mkutano huo, Mkosamali na Machali, walitoa tuhuma nzito kwa wakuu wa Wilaya ya Kibondo na Kasulu.

Kwa upande wa Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Dani Makanga, anatuhumiwa anafanya ubaguzi wa kikabila, hivyo anaruhusu wafugaji kuharibu mashamba ya wakulima wa Kagerakanda.

Wakati hayo yakisemwa kuhusu Makanga, Mkosamali alimtuhumu Mwamoto kuwa anataka kuhamisha isivyo halali Kijiji cha Nduta, ambacho wananchi walikabidhiwa baada ya kambi ya wakimbizi kufungwa katika eneo hilo.

“Mwamoto anataka kuwahamisha wakazi wa Nduta, lakini yeye mwenyewe tayari amejiorodhesha na watu wengine kujipatia eneo la ekari 73 katika kijiji hicho, sasa kwanini anafukuza wananchi hao na yeye anataka kujimilikisha eneo hilo bila kufuata utaratibu?

“Huu sio utawala bora, DC kujichukulia eneo kubwa katika makazi ya wanakijiji, tena sasa yeye na wana CCM wenzake wameanzisha ufugaji wa nyuki katika maeneo karibu na Shule ya Msingi Ndutu, jambo linaloleta usumbufu kwa wanafunzi wa shule hiyo,” alisema.

Kwa upande wake, Mbunge wa Kigoma Kusini, Kafulila, ameendelea kuwaambia wananchi juu ya ushahidi wake kuhusu suala la tuhuma za wizi katika akaunti ya Tegeta Escrow, huku akieleza sababu zake ni kwanini anataka Bunge lichunguze badala ya mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali na ofisi hiyo.

Related

Siasa 910546512523897268

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item