jaridahuru

Mitandao

ELIMU: WANAFUNZI KATIKA SHULE MBALIMBALI WAHIMIZWA KUSOMA MASOMO YA SAYANSI

 



WANAFUNZI wa shule mbalimbali nchini wametakiwa kujifunza masomo ya sayansi kutokana na umuhimu wake katika ugunduzi wa vitu ili kusaidia taifa kimaendeleo.

Imeelezwa kuwa idadi kubwa ya wanafunzi na walimu hukimbia masomo hayo na kusababisha watu kuamini ni magumu hasa kwa jinsi yanavyofundishwa.

Akitoa rai hiyo jijini Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Shirikisho la Wanasayansi Chipukizi (YS), Dk. Gozibert Kamugisha, alieleza kuwa taifa linakabiliwa na changamoto ya wataalamu wa masomo hayo, hivyo kusababisha kutofikia hatua ya kugundua vitu kama ilivyo kwa nchi nyingine.

Kamugisha alisema kuwa idadi kubwa ya wanafunzi na walimu wanashindwa kujua jinsi ya kujifunza masomo hayo hatimaye kuchangia ongezeko kubwa la upungufu wa wasomi kwenye sekta ya sayansi.

“Wanafunzi wengi wanajifunza sayansi kwa njia ya kukariri na sio vitendo, hivyo kuna tija tubadilike ili nchi yetu iendane na mifumo mipya inayoendana na mabadiliko ya dunia, hasa kwa vitendo,” alisema Kamugisha.

Alisema kuwa miongoni mwa masomo ambayo yanakimbiwa ni Hesabu, Fizikia, Biolojia, Kemia na Sayansi ya Jamii, hivyo kupunguza idadi ya ugunduzi wa vitu mbalimbali vinavyofanywa na watu wengine duniani.

Hata hivyo, Kamugisha alifafanua kwamba, katika kutumia njia za kuwavutia wanafunzi na walimu kupenda masomo hayo, shirikisho lao limekuwa likiandaa mashindano kila baada ya mwaka, lengo likiwa kushindanisha shule mbalimbali ili kujifunza masomo hayo kwa njia ya vitendo.

Related

Habari Mpya 1574522120609142900

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item