JAMII: SAKATA LA MUME WA FLORA MBASHA LAMGEUKIA GWAJIMA, AUZA MALI ZAKE NA KUIKIMBIA NCHI
https://jaridahuru.blogspot.com/2014/07/jamii-sakata-la-mume-wa-flora-mbasha.html
MBASHA akiwa na Mkewe FLORA
Kufuatia sakata la Flora Mbasha na mumewe likumuhusisha moja moja kiongozi wa kiroho Mchungaji Gwajima, habari tulizozipata ni kwamba mchungaji huyo amekimbia nchi….
Habari
toka chanzo cha kuaminika kilichopo ndani ya kanisa la
mchungaji huyo ni kuwa Gwajima hivi sasa ameshauza karibia
robo tatu ya mali zake na kwamba moja kati ya magari yake
ya kifahari huenda likanunuliwa na mwanamuziki Diamond.
“Jamaa
hivi tunavyoongea anaweza akawa ameshatoroka tayari, maana hili
sakata limeanza kumwendea hovyo na wiki iliyopita kuna madalali
walikuja hapa wakiitaka gari yake aina ya Hammer, wakidai kuwa
inataka kununuliwa na mwanamuziki Diamond,” kilisema chanzo cha
habari hii.