AFYA: EBOLA YAZIDI KUINYEMELEA AFRIKA MASHARIKI, FAHAMU JINSI YA KUJIKINGA NA EBOLA NA MADHARA YAKE
https://jaridahuru.blogspot.com/2014/07/afya-ebola-yazidi-kuinyemelea-afrika.html
Mgonjwa wa EBOLA |
Ebola ni ugonjwa hatari unaosababishwa na kirusi kiitwacho ebola. Kirusi hicho ni moja kati ya familia ya virusi watatu toka katika familia ya filoviridiae.
Zipo aina tano za kirusi cha ebola ambao nao ni
bundibugyo ebolavirus (BDBV), zaire ebolavirus (EBOV), reston ebolavirus
(RESTV), sudan ebolavirus (SUDV) na tai forest ebolavirus (TAFV).
Aina hizo tatu za virusi, yaani BDBV, EBOV na
RESTV, ndiyo inayongoza kwa kusababisha mlipuko wa ugonjwa huo barani
Afrika. Wengine wanapatikana nchi za Asia, yaani Ufilipino na Thailand
na mpaka sasa hakuna taarifa za kusababisha vifo.
Kwa mara ya kwanza ugonjwa huu uliripotiwa kutokea
mwaka 1976 katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Hatari ya
mgojwa kupoteza maisha ni asilimia 90. Watu ambao wako katika hatari ya
kupata ugonjwa huo ni jamii inayoishi karibu na jamii ya wanyama au watu
walioathirika.
Pia uwepo katika mazishi ya wagonjwa wa ebola wakati wa shughuli za kuzika na kugusana na majimaji ya mgonjwa aliyekufa.
Unavyoambukizwa na kuenea
Chanzo cha ugonjwa katika makundi yetu ni mtu
mmojawapo kugusana na damu au majimaji ya wanyama waliombukizwa, ambao
mara nyingi ni nyani, sokwe, tumbili na popo. Inaaminika kuwa popo
wanaopenda kula matunda, wanaeneza ugonjwa huo bila wao kuaathirika.
Katika jamii yetu ugonjwa huu huweza kuambukizwa
kutoka mtu mmoja mwenye maambukizi kwenda kwa mwingine baada ya kugusana
na damu au maji maji kupitia michubuko au majeraha juu ya ngozi.
Watu walio na maambukizi na wakapata nafuu bado
wanaweza kuwaambukiza wengine kwa zaidi ya miezi miwili, pia wanaweza
kuwambukiza watu wengine kwa njia ya kujamiana.
Dalili za ugonjwa
Jina jingine la ugonjwa huu ni ‘ugonjwa wa kuvuja damu’. Hii ilitokana kujitokeza dalili ya kuvuja damu mwilini.
Dalili za ugonjwa huu huu huanza kujitokeza
kuanzia wiki ya pili au ya tatu tangu kugusana na damu au majimaji ya
mwilini ya mgonjwa wa ebola.
Dalili zake ni homa kali, maumivu ya koo na misuli, kichwa kuumwa na mwili kuwa dhaifu.
Baadaye dalili zingine hujitokeza baada ya ini na
figo kuanza kuathirika dalili hizo ni kama kuhisi kichefu chefu,
kutapika na kuharisha.
Uchunguzi na matibabu
Sampuli ya damu ya mgonjwa hupimwa ili kutambua
askari mwili maalumu walizalishwa na mwili kupambana dhidi ya virusi
ebola. Pia kutazama uwepo wa DNA ya virusi wenyewe.
Ugonjwa huu hauna tiba wala chanjo kama ilivyo kwa
magonjwa mengi yanayosababishwa na virusi ambayo huwa hayana dawa wala
chanjo, bali ni matibabu ya kumsaidia mgonjwa kupata ahueni ambayo ni
kama vile kuongezewa maji kwa njia ya mshipa.
Mpaka sasa hakuna kampuni wala hospitali iliyopewa leseni ya kuuza au kutengeza chanjo.
Kujikinga na kuudhibiti ugonjwa wa ebola
Ugonjwa huu unaweza kuzuia kujitokeza na kupunguza
kuenea kwa kuwachunguza wanyama walio na ugonjwa na kuwaua na kisha
kuyatupa mabaki yao.
Kuhakikisha nyama zinapikwa vizuri, kuvaa mavazi
maalumu ya kujikinga kwa wale wanaofanya shughuli za wanyama pamoja na
watoa huduma za afya
Dalili zake ni homa kali, maumivu ya koo na misuli, kichwa kuumwa na mwili kuwa dhaifu.
Baadaye dalili zingine hujitokeza baada ya ini na
figo kuanza kuathirika dalili hizo ni kama kuhisi kichefu chefu,
kutapika na kuharisha.
Uchunguzi na matibabu
Sampuli ya damu ya mgonjwa hupimwa ili kutambua
askari mwili maalumu walizalishwa na mwili kupambana dhidi ya virusi
ebola. Pia kutazama uwepo wa DNA ya virusi wenyewe.
Ugonjwa huu hauna tiba wala chanjo kama ilivyo kwa
magonjwa mengi yanayosababishwa na virusi ambayo huwa hayana dawa wala
chanjo, bali ni matibabu ya kumsaidia mgonjwa kupata ahueni ambayo ni
kama vile kuongezewa maji kwa njia ya mshipa.
Mpaka sasa hakuna kampuni wala hospitali iliyopewa leseni ya kuuza au kutengeza chanjo.
Kujikinga na kuudhibiti ugonjwa wa ebola
Ugonjwa huu unaweza kuzuia kujitokeza na kupunguza
kuenea kwa kuwachunguza wanyama walio na ugonjwa na kuwaua na kisha
kuyatupa mabaki yao.
Kuhakikisha nyama zinapikwa vizuri, kuvaa mavazi
maalumu ya kujikinga kwa wale wanaofanya shughuli za wanyama pamoja na
watoa huduma za afya