jaridahuru

Mitandao

SIASA: WAZIRI MKUU, MIZENGO PINDA ASEMA HAYAPENDI MASWALI YA PAPO KWA HAPO

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amesema hakipendi kipindi cha maswali ya papo kwa hapo, kutokana na maswali yanayoulizwa pamoja na kuwa mazuri, lakini anayajibu bila kuwa na takwimu.

Alisema hayo bungeni jana alipokuwa akijibu swali la Rajab Mbarouk Mohammed (Ole-CUF), aliyehoji kuhusu Tanzania kuwa miongoni mwa nchi zinazoendesha shughuli za serikali kwa uwazi (OGP), mpango uliozinduliwa mwaka 2011, jijini New York, Marekani. Alitaka kujua wakati mpango huo ukiingia awamu ya pili, ni nini tathmini ya serikali juu ya mpango huo.
 
"Ndiyo maana kipindi hiki sikipendi sana, swali ni zuri lakini kunitegemea kuwa nitaweza kuwa na kila jibu kwa kila swali ni ngumu. Angeniuma sikio jambo hili ningelifanyia kazi vizuri na kutoa majibu mazuri," alisema Waziri Mkuu Pinda.

Alisema mpango huo ni miongoni mwa ambayo nchi huitumia ili kufanya shughuli za serikali kuendeshwa kwa uwazi, pia Tanzania ni sehemu ya uamuzi wa msingi wa mpango wa APRM, ambao ni namna nyingine ya kulifanya taifa kuangaliwa na mtu yeyote ili kuona namna serikali inavyoendeshwa ili Watanzania waridhike na uendeshaji wa serikali.

Chini ya mpango huo, alisema serikali imeshirikiana na nchi nyingine, wadau wa maendeleo katika awamu ya kwanza na kuweka misingi ya namna ya kushirikiana.

Alisema kinachofanyika ni kuweka mpango kuhusu mambo gani yafanyike kwa uwazi.
Alisema ni kutokana na hilo, bajeti inawekwa kwenye mitandao, pia wizara zote zina utaratibu wa kutoa taarifa kwenye mitandao.

"Ndiyo maana hata Bunge katika mambo mengine hatuna ugomvi nalo, kuna mambo tunatakiwa kuweka wazi na tunafanya hivyo," alisema.

Waziri mkuu alisema ataomba itolewe kauli ya serikali kuhusu jambo hilo na hata APRM ili kuona serikali inavyoweka mambo wazi.

CHANZO: NIPASHE

Related

SIASA: ADHABU YA LOWASSA NA WENZAKE YANUKIA? NAPE AWATOLEA UVIVU, ADAI DAWA YAO NI......(SOMA HAPA)

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari leo asubuhi katika ofisi kuu ya CCM Kisiwandui Zanzibar juu ya ratiba ya mchakato wa kupata wagombea&nbs...

SIASA: UKWELI KUHUSU FRIENDS OF LOWASSA WAFICHUKA. WAJITENGENEZEA KWA SIRI MTANDAO WAO WA KIRAFIKI

Kwa kile kinachodaiwa kuwa umoja wa marafiki ulioenea zaidi Tanzania, Umoja wa Friends of Lowassa wamejikuta sasa siri zao zikiwa wazi baada ya vyanzo vyetu kugundua mtandao wao wa siri wa kuchat ya...

SIASA: SIASA SASA YAINGIA PCCB, DR. HOSEAH AIRUKA KESI YA ESCROW..AWAKANA MAWAZIRI WANAOTUHUMIWA

Dar es Salaam. Wakati wananchi wakisubiri vigogo wa serikalini na mawaziri wanaotuhumiwa kuhusika kwenye kashfa ya uchotaji fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow kufikishwa mbele ya vyombo vya umm...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item