jaridahuru

Mitandao

KITAIFA: SERIKALI YAMALIZA UGOMVI WA MASELE NA BALOZI WA UINGEREZA, MEMBE ATUMIA DIPLOMASIA

 
Siku chache baada ya Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Steven Maselle kutaka Balozi wa Uingereza nchini Dianne Melrose, ajipime kwa kile kinachodaiwa kuingilia mambo ya ndani ya nchi, Serikali imemsafisha balozi huyo ikisema imeshalimaliza suala hilo.
 
Akizungumza bungeni mjini Dodoma, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alisema kuwa alimwagiza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Membe ambaye alikutana na balozi huyo na kuzungumza naye kabla ya kuwakutanisha na Maselle na wakaafikiana kwa njia ya kidiplomasia.
 
"Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kutoa ufafanuzi kidogo kuhusu jambo hili ambalo sote tunalifahamu kuwa liliibuka hapa bungeni, ni kweli nilimwagiza Waziri Membe na akafanya kazi ya kuwakutanisha na kuwasuluhisha wawili hawa na kwa kweli walishalimaliza kwa hiyo naomba tusiliendeleze tena," alisema Pinda.
 
Alitoa kauli hiyo kutokana na mwongozo ulioombwa na mbunge wa Viti Maalumu, Suzana Lyimo aliyetaka kauli ya Serikali kuhusu tuhuma dhidi ya balozi huyo nchini Tanzania.
 
Akizungumza katika sherehe za siku ya kuzaliwa ya Malkia Elizabeth wa Uingereza zilizofanyika nyumbani kwa balozi huyo Dar es Salaam hivi karibuni, Waziri Membe alisema hakuna mgogoro wowote wa kidiplomasia utakaowekwa na Tanzania dhidi ya balozi huyo kutokana na uhusiano wa kina uliopo baina ya nchi hizo mbili.
 
"Tumeshatuma watu nchini Uingereza kupeleka masikitiko yetu na kuomba radhi kutokana na kauli iliyotolewa bungeni. Hii ni kutokana na uhusiano mzuri tulionao Uingereza na Tanzania na hatutaki kuuharibu uhusiano huo," alisema Membe.
 
Membe alisema kwa kuwa Serikali haipo tayari kuharibu uhusiano kati ya nchi hizo mbili, Waziri Mkuu Mizengo Pinda atalizungumzia suala hilo hivi karibuni bungeni, ili kumhakikishia balozi huyo kuwa hana tuhuma za kujibu.
 
Mei 30 mwaka huu, Waziri Maselle alimlipua balozi huyo wakati akichangia hoja iliyotolewa na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila(NCCR-Mageuzi) bungeni iliyoihusisha Uingereza na urejeshwaji wa Sh76 bilioni za chenji ya Rada.
 
Akichangia hoja hiyo, Maselle alimshutumu Balozi wa Uingereza kuhusika na kuratibu vikao jijini Dar es Salaam na Dodoma kinyume cha taratibu na hadhi ya kidiplomasia.
 
Alidai kuwa balozi huyo amekuwa akihusika katika kusambaza ujumbe mfupi unaodaiwa kutaka kukwamisha Bajeti ya Nishati na Madini pamoja na kuwashawishi marafiki wa kimaendeleo wasitishe misaada ya kibajeti kwa Tanzania.
 
Katika maelezo yake, Membe alisema tuhuma zilizotolewa hazina ukweli wowote na ni lazima zitolewe ufafanuzi ndani ya Bunge ili kudumisha urafiki wa nchi hizo mbili.
 
"Kama kauli hiyo ilivyotolewa bungeni kumshutumu balozi, hali kadhalika tutahakikisha tunaomba msamaha kwa kile kilichotamkwa dhidi ya balozi. Uchunguzi umefanyika na tumegundua kuwa hakuna tuhuma zozote zenye ukweli dhidi yake," alisema.

Related

KITAIFA: MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA YALIA NA VIONGOZI WA DINI NA MITANDAO YA KIJAMII

Dar es Salaam.Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imewataka viongozi wa dini kutumia nafasi kukemea juu ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii kwa waumini wao na kuelimisha madhara yanayow...

KITAIFA: POLISI AJIUA KWA KUJIPIGA RISASI HUKO SINGIDA, AANDIKA UJUMBE MZITO NA KUUACHA. UNAHUSU VURUGU ZA DAR??

 Mnamo tarehe 02/02/2015 majira ya saa 10.35hrs askari no.G.4228PC. ALOYCE ambaye alikuwa dereva wa OCD-MANYONI alifika kwa armoury keeper na kumuomba amkabidhi silaha kwani anasafari na OCD...

GARI LATEKETEA KWA MOTO LIKIWA KWENYE FOLENI JIJINI DAR.

Saa chache zilizopita katika Barabara ya Kawawa, Ilala Dar imetokea ajali ya moto, gari ndogo imewaka moto lakini hakuna mtu aliyeathirika kutokana na tukio hilo. Mmiliki wa gari hilo&nbs...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item