jaridahuru

Mitandao

JAMII: VICKY KAMATA AFUNGUKA KUHUSU MADAI YA MCHUMBA WAKE KUWA MUME WA MTU NA KUZUILIWA NDOA YAKE

 Mwanamuziki wa zamani na mbunge Vicky Kamata baada ya ndoa yake kudaiwa kuzuiliwa kufungwa kutokana na kudaiwa mwanaume aliyetaka kufunga naye ndoa ana ndoa nyingine, amefunguka kwa kudai kuwa hizo zilikuwa ni habari za kutungwa na hazikuwa na ukweli wowote.
 
Vicky ameiambia amplifaya ya Clouds fm jana kuwa maneno mengi ambayo yalikuwa yanazungumzwa kuhusu ndoa yake kutofungwa yalikuwa yametengenezwa na watu.
“Kweli ni maradhi kama ambavyo ilitangazwa wakati huo, lakini pamoja na hayo mimi bado nasema mungu alikuwa hajapanga ,alikuwa hajaruhusu kuwa tarehe 24 mwezi wa tano iwe siku wa kufunga ndoa.
 
“Mimi kama binadamu na mwenzangu tulipanga lakini mungu alipanga vinginevyo , kwaiyo siku zote mapenzi ya mungu huwaga yanatimia siyo mapenzi ya binadamu.
 
“Ni kweli alishawai kufunga ndoa lakini ninachofahamu mimi ni kwamba waliachana kihalali kabisa kwa divorce ya mahakama ya Kinondoni mwaka 2012 na mimi siyo mtoto mdogo kwamba ninaweza mpaka nikafikia hatua hiyo bila kuwa nimemchunguza huyo mtu.
 
“Kuhusu swala la kwamba alikuwa na mke wake , mke wake alikwenda kuzuia Kanisani sijui alikuja Bungeni, yale yalikuwa tu ni maneno ambayo yalitengenezwa na baadhi ya watu kwa interest zao ,lakini siyo kwamba nilikuwa nimeingilia ndoa ya mtu hata kidogo, kwa sababu ata huyo mke wa kwanza wa huyo aliyekuwa mchumba wangu aliongea na vyombo vya habari akasema mimi sijaenda Dodoma wala sijaenda kuzuia harusi.
 
“Kwaiyo maneno yaliyokuwa yamezagaa ,sijui mke wake amezuia yalikuwa ni maneno ya kutengenezwa na watu tu kwa nia zao wenyewe lakini siyo kweli.
 
vicky
 
“Kuhusu kwamba hajulikani alipo mimi hilo siwezi kumjibia, mimi nafahamu kwamba yupo na anaendelea na shughuli zake kama kawaida, kama ambavyo mimi naendelea na shughuli zangu kama kawaida, tunawasiliana, yani cha kufahamu tu kwamba ndoa haikufungwa basi.
 
“Hata kama kuna mkono wa binadamu katika jambo hilo mimi naamini mungu ndo mwenye mamlaka na Mungu ndiyo mwenye kupanga mambo, kwaiyo kama Mungu alikuwa anataka hiyo harusi ifugwe ata kama kungekuwa na binadamu mwingine hataki bado ingefungwa…
 
“Kwaiyo mimi sitaki kuamini sana kwamba kuna waheshimiwa wabunge wenzangu wamechangia kwa kiasi kikubwa kwamba ndoa ile isifungwe, mimi ninaamini ni mapenzi ya Mungu tu yametimizwa kwa staili hiyo” Alisema Vicky

Related

JAMII: MZINDAKAYA AONJA CHUNGU YA MAGUFULI, ANYANG'ANYWA NYUMBA 12 NA WIZARA YA UJENZI

WIZARA ya Ujenzi imeinyang’anya Kampuni ya Agriculture and Animal Food Industries Ltd (Saafi), inayomilikiwa na mwekezaji mzalendo na mwanasiasa mkongwe, Dk. Chrisant Mzindakaya nyumba 12 za umm...

AJALI: DEREVA APONA KUTOKA KWENYE AJALI MBAYA BAADA YA GARI LAO KUANGUKIWA NA KONTENA ATOKA MZIMA

This is the incredible moment two people were pulled alive from a car that had been almost entirely flattened by a shipping container falling on top of it. Firefighters arriving at the scene in Qin...

AFYA: EBOLA YAZIDI KUINYEMELEA AFRIKA MASHARIKI, FAHAMU JINSI YA KUJIKINGA NA EBOLA NA MADHARA YAKE

Mgonjwa wa EBOLA Ebola ni ugonjwa hatari unaosababishwa na kirusi kiitwacho ebola. Kirusi hicho ni moja kati ya familia ya virusi watatu toka katika familia ya filoviridiae. ...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item