jaridahuru

Mitandao

JAMII: MHESHIMIWA JOHN KOMBA MBUNGE CCM APIGA PICHA ZA URODA, ZASAMBAA MTANDAONI, AKANA KUHUSIKA


Picha zinazomwonyesha mh. Captain John Komba zenye mapozi tofauti na mabinti tofauti zimeanza kusambazwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii hapa Tanzania.

Kuna picha nyingine nyingi lakini kutokana na maadili hatuwezi kuziweka hadharani; hizi ni baadhi tu

Kuhusiana na hizi picha 2 zilizoenea kwenye mitandao ya kijamii kuznia asubuhi ya leo, zikimuonyesha Mheshimiwa Mbunge huyo wa CCM Kapteni John Komba akiwa kwenye mahaba na Mwanadada mmoja anayeishi Kinondoni.

Mbunge huyo amesema kwamba picha hizi zimetengenezwa na maadui wake wa kisiasa na kwamba yeye sio Kiongozi wa hovyo hovyo namna hiyo.

Kapteni Komba amesema kwamba anawakaribisha wataalamu wa Picha na Mitandao kutihibitisha ukweli wa picha hizo zinazoonyesha Mwana-Dada akiwa na kipande cha khanga tu huku Mbunge huyo akiwa pembeni yake akionyesha kutokuwepo kabisa kwenye Mahaba yanayotakiwa kuwa yanaendelea baina yao.

Mbunge huyo ameuliza zaidi iweje awe kwenye mapenzi kama picha zinavyo onyesha halafu awe na nguo zake zote huku msichana akiwa na khanga tu?

Kapteni Komba amesema kwamba kama kweli Taifa hili limefikia hapa pa kuchafuana namna hii kisa mitizamo tofauti ya kisiasa ya namna ya kuongoza Taifa letu basi kama Taifa tumefikia pabaya sana.

Mbunge huyo amemalizia kwa kusema kwamba wale wote wanaomuamini kama Kiongozi shupavu wa Taifa, wasikatishwe tamaa na wajinga wachache wenye mawazo ya kitumwa ambao wanadhani wanaweza kummaliza kisiasa kwa kumtengenezea picha chafu kama hizi picha 2 za leo!

Related

Kitaifa 3844877082182966771

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item