jaridahuru

Mitandao

AFYA: MGONJWA ATOKA HOSPITALI NA UGONJWA MWINGINE, YAMBIDI AKIMBILIE KWA MGANGA WA KIENYEJI




Geita. Mgonjwa aliyepooza nusu mwili ambaye alikuwa amelazwa Hospitali ya Rufani Bugando Mwanza, amejikuta katika hali ngumu baada ya kuruhusiwa kurudi nyumbani akiwa na kidonda kikubwa sehemu ya makalio kilichotokana na kulala kwa muda mrefu kitandani bila kugeuzwa.
Joseph Luhogola (38), ambaye amepooza mwili kuanzia usawa wa kifua hadi miguuni, amelazimika kwenda kwa mganga wa Kienyeji kutumia miti shamba kutibiwa ugonjwa unaomsumbua.
Luhogola, mkazi wa Kijiji cha Mganza, wilayani Chato, mkoani Geita, licha ya kuruhusiwa kutoka hospitalini, ndugu na jamaa waliokuwa wakimuuguza hawakutambua kama alikuwa na kidonda kikubwa sehemu hiyo.
Ndugu zake akiwamo mkewe, Kefline Kafaransa (36) hawakutambua kama alikuwa kwenye hali hiyo hadi walimpofika nyumbani kwa mdogo wake, baada ya kumvua nguo ndipo walipobaini hali hiyo.
Hali hiyo ilisababisha mdogo wake, Mustafa Luhogola (36) mkazi wa Nyankumbu mjini Geita kupoteza fahamu kwa dakika 35 kutokana na mshtuko baada ya kuona kidonda hicho.
Luhogola alifikishwa Bugando Aprili 22 mwaka huu, baada ya kupata ajali iliyotokana na gari dogo la kubeba abiria kupinduka Kijiji cha Lubambagwe, Chato.
Akizungumza kwa shida huku akiwa amelazwa chumba maalumu cha mganga wa kienyeji, Luhogola alisema baada ya kutokea ajali hiyo alipoteza fahamu na kujikuta akiwa Bugando.“Kwa sasa sijitambui kuanzia sehemu ya kifuani hadi miguuni, kidonda kinachosemwa kwenye makalio sikitambui ingawa nakumbuka maelekezo ya wauguzi kunitaka nilale chali bila kugeuzwa,” alisema Luhogola.
Mkurugenzi wa Hospitali ya Bugando, Dk Charles Mjinge alipoulizwa juu ya mgonjwa huyo alisema hajui iwapo kidonda hicho kilisababishwa na ajali au la na kwamba, inawezekana kulala muda mrefu kutokana na kupooza ndiyo chanzo.“Ili kuweza kueleza haya mgonjwa aje tuone, tutafute jalada lake tuweze kufuatilia kilichotokea, siyo kawaida mtu kumruhusu akiwa na kidonda kikubwa kama unavyokielezea,” alisema Dk Majinge na kuongeza:“Labda walimweleza mgonjwa hawakuwaeleza ndugu, ndiyo maana hawakujua kama ana hali hiyo, sasa mwambie aje na nyaraka za taarifa zake, lakini kuna tatizo la watu kama hao wamekuwa wakiomba ruhusa ili waende kwa waganga wa kienyeji hasa hao wenye kupooza mwili.”
Mganga wa kienyeji anena.
Mganga wa kienyeji ambaye anamtibu Luhogola, Paulo Chasama alisema yeye ni mtalaam wa kutibu mifupa iliyovunjika na watu waliopooza mwili tangu mwaka 1997 alipoanza kazi.
Kuhusu mgonjwa huyo, Chasama alisema uhakika wa kupona ugonjwa wa kupooza upo na kwamba, ndani ya mwezi mmoja atakuwa kwenye hali nzuri isipokuwa tatizo kubwa ni kidonda.
“Walichokosea huko hospitali ni kule kumlaza chali kila siku bila kumgeuza, hali iliyosababisha kuwa na kidonda kama hiki, lakini suala la kupooza halitachukua muda mrefu atapona,” alisema

Related

Jamii 1001042725067182241

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item