jaridahuru

Mitandao

MICHEZO: SEEDORF AONESHWA MLANGO WA KUONDOKEA, FILIPO INZAGHI SASA KUINOA AC MILAN


AC Milan wamemfukuza kazi Kocha Clarence Seedorf na kumpa kazi hiyo Filippo Inzaghi.
Seedorf amefukuzwa kazi ikiwa ni pungufu ya miezi mitano tu tangu achaguliwe kushika nafasi hiyo kwa klabu inayocheza Ligi Kuu ya Italia – Serie A.
Mdachi huyu mwenye umri wa miaka 37 alipewa mikoba kwenye klabu aliyochezea kwa miaka 10 tangu 2002.

Inzaghi naye ni mkongwe aliyechezea AC Milan lakini hajapata kufundisha timu iliyo katika ligi kuu. Alikuwa akifundisha timu ya vijana chini ya miaka 19 y AC Milan.(P.T)

Inzaghi (40) amepewa mkataba wa miaka miwili na ameajiriwa baada ya mmiliki wa klabu na rais wake, Silvio Berlusconi kusema Ijumaa iliyopita kwamba Seerdof ni sehemu ya walioshindwa kazi hapo San Siro. Berlusconi ni waziri mkuu wa zamani wa Italia na ni mfanyabiashara bilionea anayemiliki pia vyombo vya habari.

Enzi za kusakata kwake soka, Inzaghi alichangia kwa kiasi kikubwa Timu ya taifa ya Italia kutwa ubingwa wa dunia 2006, makombe mawili ya Uefa na makombe matatu kwa AC Milan katika Serie A.

Seedorf alichukua nafasi ya kocha aliyemtangulia, Massimiliano Allegri aliyefukuzwa kazi kutokana na kuanza vibaya msimu wa Ligi Kuu 2013/14. Aliajiriwa akitoka kuchezea klabu ya Botofago ya Brazil, ambapo inaelekea alitundika daluga makusudi kwa kazi hiyo.

Wachambuzi wengi wa masuala ya soka walikuwa na wasiwasi juu ya uteuzi wake na iwapo angedumu kwenye kazi hiyo na kweli amefukuzwa baada ya ligi kumalizika.
Alipoajiriwa AC Milan kama kocha, Seedorf alisema alidhamiria kuirejesha klabu kwenye heshima iliyokuwa nayo awali

AC Milan walmfukuza Allegri baada ya kufungwa na vibonde Sassuolo 4-3 Januari mwaka huu. AC Milan wamekuwa mabingwa wa Italia mara 18 na alipofukuzwa walikuwa nafasi ya 11 na wamemaliza ligi wakiwa nafasi ya nan echini ya Seedorf.
Chanzo:http://www.tanzaniasports.com/

Related

BURUDANI: NEW VIDEO RELEASED JUX - SISIKII

Hii ni video iliyokuwa inazungumziwa sana baada ya kusambaa kwa picha ambazo zilikuwa behind the scene zikimuonyesha Vanessa Mdee na Jux ambao kumekuwa na story kw...

BURUDANI: UNAJUA KUWA UKIWA MREMBO NI ZAIDI YA DEGREE? MASOGANGE AHONGWA GARI AINA YA BENZ..UPOOO?!!

Mrembo Agness Masogange Ambae hivi karibuni aliukana Uraia wa Tanzania na kuchukua Uraia wa South Africa ni ni kama Ameunza Mwaka Vizuri Baada ya Kupost meseji alizochat na mpenzi wake zikion...

BURUDANI: DIAMOND APATA SHAVU LINGINE TENA! ACHAGULIWA KUTUMBUIZA TUZO ZA MWANASOKA BORA CAF

  Msani Nasib Abdul 'Diamond' amechaguliwa kuwa mmoja wa wasanii watakaotumbuiza kwenye hafla ya utoaji tuzo za mwanasoka bora Afrika 2014. Diamond atatumbuiza katika tuzo hizo ambazo w...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item