jaridahuru

Mitandao

JAMII: TAKUKURU YAINGILIA KATI MGOGORO WA ARDHI WA SHULE YA MSINGI WERENI MOSHI

Moshi. Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (Takukuru), imeanzisha uchunguzi wa mikataba ya kubadilishana shamba kati ya Shule ya Msingi Wereni na mfanyabiashara, Thom Ndesamburo.
Mfanyabiashara huyo anayemiliki vitega uchumi kadhaa, aliingia mkataba wa kubadilishana shamba na uongozi wa shule hiyo iliyopo Kata ya Kibosho Magharibi, Wilaya ya Moshi Vijijini.
Thom ni mtoto wa Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo anayemiliki Hoteli ya Snow View, vituo vya mafuta na maduka ya kuuza vifaa vya ujenzi.
Taarifa zinadai kuwa, baadhi ya viongozi wa shule hiyo na wale wa Kijiji cha Umbwe Sinde, walifanya udanganyifu katika mkataba huo na hilo limeisukuma Takukuru kufanya uchunguzi.
Habari zinadai kuwa Takukuru inaendelea kuwahoji baadhi ya viongozi wa shule hiyo na viongozi wa Kijiji cha Umbwe.
Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Kilimanjaro, Lawrence Swema alithibitisha kuhojiwa viongozi hao, lakini akakataa kufafanua zaidi kwa madai ya sheria kumzuia kuzungumzia jambo lililo kwenye uchunguzi.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Onesmo Kinyaiya alipotafutwa na gazeti hili jana, hakuwa tayari kuzungumza lolote zaidi ya kusema alikuwa ofisi za Takukuru.
Akizungumzia suala hilo, Ndesamburo alisema alifuata taratibu zote na nyaraka husika anazo

Related

Jamii 1865021382105436862

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item