jaridahuru

Mitandao

SIASA: MNYIKA SASA AMKALIA KOONI RAIS, ATAKA ATEKELEZE AAGIZO LA WANANCHI WA UBUNGO


Mbunge wa jimbo la Ubungo, Jon Mnyika, amemtaka Rais Jakaya Kikwete kutekeleza ahadi ya kuwapatiwa wananchi wake huduma ya maji aliyoitoa mwaka mmoja uliopita.

  Ametoa wito huo jana alipokuwa akifungua semina ya kuwajengea uwezo viongozi wa ngazi mbalimbali wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kutoka kata zote 14 za jimbo hilo.

  “Namuomba Rais Kikwete awaambie wananchi wa Ubungo ni lini kikao alichokiahidi Machi mwaka jana kati yake, mimi, Dawasa na Dawasco kitafanyika ili kuwaondolea kero wapigakura hawa. Afanye hili ili asionekane muongo mbele ya wananchi hawa,” alisema.

  Mnyika alieleza pia kuwa mradi wa ujenzi wa mabomba makubwa ya maji uliokuwa unatekelezwa na kampuni ya Kichina hauna tija kwani mabomba hayo hayatoi maji kama ilivyokusudiwa na akaitumia nafasi hiyo kuhoji kama hilo nalo ni miongoni mwa faida za ziara ya hivi karibuni ya rais nchini huko.

  Alisema “ni matumizi mabaya ya rasilimali za nchi kama mradi unaweza ukatekelezwa pasipokuleta matunda yaliyokusudiwa. Rais awaeleze wananchi kama aliwauliza Wachina juu ya kampuni iliyotekeleza mradi huo.”

   Alifafanua kuwa ombi la kukutana na Rais lilitolewa na wananchi wa kata ya Goba na limeungwa mkono na wananchi wa jimbo zima kupitia viongozi wao waliohudhuria semina hiyo inayowajengea uwezo na kuwaelimisha juu ya maadili na misingi ya chama, nafasi ya chama katika kuchangia maendeleo pamoja na kuwahamasisha kushiriki katika uchaguzi wa serikali za mitaa.

  Washiriki wa semina hiyo walimhakikishia naibu katibu mkuu huyo wa Chadema bara kuwa tayari wameandaa wagombea katika kila kata ambao watatoa upinzani wa kutosha dhidi ya Chama Cha Matinduzi (CCM) na kuondoa mazoea ya kuwa na maeneo yasiyokuwa na upinzani.

Related

Siasa 622550791727903258

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item