jaridahuru

Mitandao

SIASA: WANACHAMA WA CHADEMA WAKAMATWA NA POLISI MOROGORO KWA KUFANYA MAANDAMANO BILA KIBALI

Wafuasi wa Chadema wakamatwa kwa maandamano Morogoro.



Wanachama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wapatao 8 wamekamatwa katika mkoa wa Morogoro kwa kufanya maandamano pasipo kupata kibali cha jeshi la Polisi.

Wanachama waliokamatwa ni pamoja na Witnes Makoyola ambaye ni katibu wa Chadema tawi la kiwanja cha ndege, Shukuru Makamba, Maria Lissu, Hussein Hassan pamoja na Odwin Peter mkazi wa kiwanja cha ndege.

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoani Morogoro Leonard Paul wanachama hao walitenda tukio hilo katika maeneo ya mtaa wa Konga.

Ameongeza kwamba jeshi hilo liliwazuia wanachama kuandamana lakini hawakutii agizo hilo ambapo jeshi la Polisi liliwatawanya kwa mabomu ya machozi sambamba na kuwakamata watuhumiwa hao ambapo watafikishwa mahakamani muda wowote kuanzia sasa.

Related

Siasa 3956661240640200055

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item