jaridahuru

Mitandao

BURUDANI: STEVE NYERERE AONGELEA ISHU YAKE YA USHOGA, ASEMA HAPENDI WATU WANAOMFUATILIA MAMBO YAKE




MWENYEKITI wa Bongo Movie, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’, amekerwa na alichosema uzushi dhidi yake kwamba ni shoga.

Kupitia ukurasa wake wa facebook, msanii huyo alisema anachukizwa na kasumba ya baadhi ya watu kufuatilia mambo binafsi ya watu.

“Napenda kuchukua fursa hii kusema machache, kama ‘nitamboa’ mtu naomba samahani.
“Najua binadamu tumezaliwa tofauti sana, kuna wale wanaoogopa dhambi na wengine wanaopenda dhambi.

“Nimepata taarifa humu kwenye mitandao yetu ya kijamii, kwamba kuna binti anaitwa Zainab ananichafua akiniandika mambo ambayo hayana tija kwangu, kwamba mimi shoga, ana uhakika?
“Nimecheka sana kupata hizi taarifa, nataka kuwaambia ndugu zangu kuwa mti wenye matunda ndio upigwao mawe, namkanya mara moja aache kwani naamini anapoteza muda tu, habari hizi sio za kweli kabisa,” alisema.

Msanii huyo mwenye kipaji cha kuigiza sauti za watu wengine hasa maarufu, aliongeza kuwa anamtakia kila la heri kwa jambo alilomtendea na anamuachia Mungu, ila yeye ana mke na watoto, hivyo anajisikia vibaya sana kuzushiwa.

Aliongeza kuwa anajua wanaamua kumchafua baada ya kujionyesha wazi kwenye siasa.
“Watu wananitumia meseji mbaya, eti mimi nimetumwa na viongozi, mara sijui ni shoga, hakuna mambo hayo, nawataka Watanzania wajue hayo ni mambo ya uzushi, sijui hata yametoka wapi,” alisema.

Related

Habari Mpya 5284210905545538064

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item