jaridahuru

Mitandao

BNGENI: DR. KASHILILLAH AWASIHI WABUNGE WANAWAKE KUSHIRIKI KATIKA MAAMUZI MUHIMU


Arusha. Wanawake barani Afrika wametakiwa kushiriki katika uamuzi ili kufikia malengo waliyoyakusudia.
Katibu wa Umoja wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola wa Kanda ya Afrika (CPA), Dk Thomas Kashilillah aliyasema hayo jana alipozungumza katika Kikao cha Kamati ya Wabunge Wanawake wa jumuiya hiyo kilichojadili masuala mbalimbali ikiwamo kuwawezesha katika uwakilishi.
Dk Kashilillah ambaye pia ni Katibu wa Bunge la Tanzania alisema umefika wakati wanawake wa Afrika kushiriki katika shughuli za kikanda ili kujijengea uwezo.
“Sasa ni wakati mwafaka kwa wanawake kwenye kanda yetu kushiriki katika semina na makongamano mbalimbali yatayowajengea uwezo zaidi katika shughuli zenu,”alisema Dk Kashilillah.
Aliwataka wanawake kuanzisha jukwaa lao litakalowawezesha kujadili maslahi yao ambalo linaweza kuwakutanisha mara mbili kwa mwaka ili kutimiza malengo hayo.
Mjumbe wa kamati hiyo kutoka hapa nchini, Anna Abdallah alisema kupitia mipango ya aina hiyo ya uwezeshaji wanawake, Tanzania imeweza kupiga hatua kubwa kwa kuwajengea wanawake uwezo wa kuongoza na kuingia katika vyombo mbalimbali vya uamuzi.
Alisema Tanzania ni moja ya nchi zilizo na uwakilishi wa kutosha wa wanawake katika ngazi za uongozi na ushiriki wa nafasi walizonazo umekuwa na manufaa.

Related

Habari Mpya 121921585650501809

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item