jaridahuru

Mitandao

SIASA: MAKAMU MWENYEKITI CCM, PHILIP MANGULLA AIFAGILIA UKAWA. ASEMA UKAWA ITAWAPA NGUVU ZAIDI UPINZANI



Dar es Salaam. Makamu Mwenyekiti wa CCM, Philip Mangula amevipongeza vyama vya upinzani kwa kuungana na kuunda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) akisema hatua hiyo itawafanya kuwa na nguvu zaidi.
Katika kuonyesha kufurahishwa na hatua hiyo ya upinzani, Mangula alihitimisha salamu zake wakati wa ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa sita wa CUF jana, kwa kusema: “Ukawa oyee,” na kuwafanya wajumbe kumshangilia kwa nderemo na vifijo.
Mangula alisema umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu: “Ninawapongeza kwa kuungana na kuunda Ukawa, hata Mwalimu Julius Nyerere aliwahi kusema angependa kitokee chama cha upinzani chenye nguvu ambacho kinaweza kushindana na CCM ili kuwaletea wananchi maendeleo.”
Msimamo
Wakizungumza katika mkutano huo viongozi wa Ukawa walisisitiza kwamba hawatarejea katika Bunge Maalumu la Katiba hadi yafanyike mabadiliko ya kujadili Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba badala ya kujadili rasimu ya CCM.
Msimamo huo ulitolewa kwa nyakati tofauti na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Makamu Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Leticia Mosole.
Akifungua mkutano huo, Profesa Lipumba alisema: “Kamwe haturudi bungeni kujadili Rasimu ya Katiba ya CCM, bali tutarudi kujadili Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba, huo ndiyo msimamo wetu.
“Rais Jakaya Kikwete afahamu msimamo wetu mapema ili aweze kuchukua hatua za kunusuru mchakato huu, yeye ndiye atakayeamua kama turudi au tusirudi,” alisema huku akishangiliwa na wajumbe ambao kila aliposema Ukawa… wajumbe waliitikia ‘tumaini letu’.
Katika salamu zake, Mbowe alimtaka Mangula kumpelekea salamu Rais Kikwete kwamba Ukawa hawarudi katika Bunge Maalumu la Katiba hadi madai yao yatimizwe.
“Kwa kuwa Mzee Mangula upo hapa leo tunakuomba  uwapelekee salamu wenzako, waeleze kwamba haturudi bungeni, waeleze kwamba huo ndiyo msimamo wetu usioyumba,” alisema na kuongeza:
Mosole licha ya kuunga mkono hoja hiyo akisema ndiyo msimamo wa chama chake, aliukosoa uchaguzi wa CUF: “Nimekuja hapa lakini nashangazwa kwa nini hakuna wanawake wanaogombea nafasi za juu za uongozi wakati wapo wenye uwezo, naomba mbadilike.”
Kupokezana vijiti
Wakati Profesa Lipumba na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad wakitetea nafasi zao, Makamu Mwenyekiti wa CUF, Machano Hamis Ali alitangaza kuachia ngazi akisema uongozi ni kama mchezo wa kupokezana vijiti.
“Sijachukua fomu za kugombea nafasi yoyote kwa sababu ya afya yangu siyo nzuri, pia nafahamu kwamba uongozi ni kupokezana vijiti.”

Related

Siasa 5288142974525931650

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item