jaridahuru

Mitandao

JAMII: MAMA WA MSICHANA WA KAZI ALIYECHOMWA NA PASI APIGA YOWE WODINI NA KUSIMAMISHA HUDUMA, ADAI MWANAWE


Kelele za vilio jana zilisimamishwa kwa muda shughuli katika Wodi ya Wanawake ya Hospitali ya Mwananyamala, Dar es Salaam baada ya mama mzazi wa msichana, Yusta Lucas (20) anayedaiwa kuteswa kwa kung’atwa na kuchomwa kwa pasi mwili mzima kumwona mwanawe kwa mara ya kwanza.

Zilikuwa dakika 10 ngumu kwa mama huyo, Modesta Simon kuamini hali aliyomkuta mwanaye aliyelazwa hospitali hapo kuuguza majeraha kutokana na kufanyiwa ukatili na tajiri yake Amina Maige.
1
Mwanamke huyo anashikiliwa katika Kituo cha polisi Oysterbay kwa tuhumu hizo na Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni Thobias Edoyeka alisema leo atafikishwa mahakamani… “Bado sijafahamu kama atapelekwa ama Kisutu au Kinondoni.”
2
Mara baada ya mama huyo kuingia katika wodi hiyo, Yusta aliyekuwa ameketi kitandani aliruka na kumkimbilia mlangoni na kilichofuata ni vilio.
Akizungumza huku akitokwa na machozi, Modesta alisema: “Jamani Amina kweli amekufanya hivi, kila nikiuliza wananiambia hujambo kumbe umeharibika hivi…”
Alisema habari za mateso na kulazwa kwa mwanaye alizipata kutoka kwa ndugu yake anayeishi Arusha…
“Alhamisi nilipata simu kutoa kwa ndugu yangu Marieta Shitindi yeye anakaa Arusha, akaniambia ameona kwenye  runinga kwamba Yusta amelazwa baada ya kupigwa na Amina ndipo nikafunga safari kutoka Tabora kuja kuhakikisha.

Amina ni mtoto wa mjomba wangu kabisa na sikuwahi kuambiwa chochote, niliamini wanaishi vizuri na sikudhani kama anaweza kulifanya jambo hili.”
3

Modesta alisema awali alikuwa na mawasiliano na mwanaye kupitia simu ya mama yake Amina ambaye wanaishi karibu, lakini hivi karibuni alianza kupata wasiwasi baada ya kila alipohitaji kuongea naye alipatiwa sababu hivyo akaomba Yusta kurudishwa na aliahidiwa angepelekwa mwezi huu.

“Aliniahidi mwezi huu atamleta Yusta nyumbani alisema anataka muda amnunulie na cherehani ili akija apate shughuli ya kufanya…” alisema.
Ofisa Muuguzi katika wodi aliyolazwa Yusta, Erica Massawe alisema hali ya binti huyo imeimarika na alisharuhusiwa kutoka tangu Ijumaa iliyopita na kwamba wanasubiri maelekezo ya Polisi na Ustawi wa Jamii kwani ndiyo wahusika wakuu.

Related

Jamii 5255773136985103259

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item