jaridahuru

Mitandao

JAMII: ASKOFU AWATAKA WATANZANIA KUTOKUBALI KUGOMBANISHWA NA WANASIASA WACHOCHEZI

 
Watanzania wametakiwa kutokubali kugombanishwa na wanasiasa  ambapo hivi sasa kumekuwepo na siasa navyama vingi ili kuepuka kuleta vurugu na kuvunja amani ambayo nchi ya Tanzania imeweza kudumuisha  amani na utulivu na kuwa nchi ya mfano katika bara la Afrika kwa  muda wa miaka hamsini badala yake wawe na msimamo nakuungana kudumisaha amani iliyopo nchini.
 
Hayo  yalisemwa mapema jana na Askofu mkuu wa makanisa ya International Evangelism Bw,Eliudi Isangya wakati wa mahafali ya 63 ya chuo cha biblia kilichopo eneo la sakila wilaya ya Arumeru mkoani Arusha yaliyofanyika chuoni hapo na zaidi ya wahitimu 79 walihitimu stashahada ya biblia amabapo ni wanafunzi kumi na moja kutoka nchini Kenya na 68 kutoka nchini Tanzania ambapo masomo hutolewa bure.
 
Alisema kuwa hivi sasa hali ya kisiasa imetawaliwa na ugomvi ugomvi wa mara kadhaan hali ambayo inahatarisha maisha ya wanaanchi na kuweza kuleta maendeleo yao badala yake amewataka wanasiasa kufanya siasa za kistaarabu na tija ili kuweza kuleta maendeleo ya katika majimbo na taifa kwa ujumla.
 
Aidha amewataka waamini wote nchini kuweza kuwa na hofu  na mungu ili kuweza kuenenda vile mungu atavyotaka kwa mapenzi mema na kumtukuza mungu ili kuwa na amani ili kuweza kuleta maendeleo badala ya kuishi kwa hofu .
Hata hiyo askofu aliwataka wahitimu hao pamoja na wahubiri kuweza kuwafundisha watu kuhusu mazingira safi kuanzia rohoni na mazingira wanamoishi ili kuweza kuepuka vitendo vyote vya kuendana kinyume na mazingira tunamoishi.
 
Awali akisoma risala ya wahitimu wenzake bw. Moses Kaaya  alisema kuwa mbali na juhudi za kupewa masomo ya biblia lakini bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali chuoni hapo ikiwemo ukosefu wa miundo mbinu chuoni hapo ,kukatikakatika kwa umeme hali ambayo inawakwamisha katika jitihada zao za kujisomea na kuweza kuwa chachu ya mabadiliko katika jamii ambapo kwa sasa kumekuwepo na kumomomyoka kwa maadili.
 
Aliongeza kuwa ukosefu wa maji umekuwa nikikwazo katika eneo hilo la chuo hali inayolazimu uongozi kufata maji mbali na kuongeza gharama za uendeshaji na kuomba wizara ya maji kupitia mamlaka ya maji mkoa wa Arusha kuweza kuwasaidia suala hilo ili kuweza kusoma kwa tija na ufanisi zaidi.
Kaaya aliongelea suala la uhamiaji haramu ambapo limekuwa tatizo sugu na kuitaka serikali kuweza kushughulika nalo na kuweza kuepuka machgafuko yanayoweza kutokea nchini.

Related

Jamii 229626705594875523

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item