jaridahuru

Mitandao

BUNGENI: ZITTO AITOLEA UVIVU SERIKALI, ASEMA KUSHUSHA PAYE TOKA ASILIMIA 13 HADI 12 HAIMSAIDII MFANYAKAZI



Dodoma. Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe amesema unafuu wa Kodi ya Mshahara (Paye), uliotangazwa na Serikali kwamba umeshuka kutoka asilimia 13 hadi 12 ni mdogo hautamsaidia mfanyakazi kubaki na fedha kwa ajili ya matumizi wala kujiwekea akiba.
Katika mchango wake wa maandishi kwa Bajeti ya Serikali jana, Zitto alisema ni dhahiri kuwa Paye ni chanzo kikubwa cha mapato ya ndani ya Serikali lakini akapendekeza kipunguzwe zaidi.
Mbunge huyo alishauri kiwango cha chini cha mshahara unaokatwa kodi kiwe Sh330,000 na kiwango cha chini cha kodi kiwe asilimia tisa.
“Kiwango hiki cha kodi pia kinawezekana kwa Serikali kuchukua hatua dhidi ya matumizi mabovu,” alisema Zitto na kuongeza:
“Kwa mfano, kwa mujibu wa Taarifa ya Mkaguzi Mkuu wa ndani wa Serikali mwaka 2013, mfumo wa kukagua utumishi wa umma umegundua kuwa jumla ya wafanyakazi wa Serikali 6,500 walikuwa wameajiriwa mara mbili kwa majina yaleyale, 2,700 mara tatu na kulikuwa na watumishi 2,500 waliokuwa wanachukua mishahara miwili mpaka mitatu kila mwezi.”
Alisema hatua ya kuondoa matumizi mabovu kutokana na kulipa mishahara hewa pia inaweza kusaidia kupunguza mzigo wa kodi kwa wafanyakazi nchini.
“Serikali hutumia wastani wa Sh360 bilioni kila mwezi kulipa mishahara na kati ya hizo Sh10 bilioni zimekuwa zikilipwa kwa watumishi hewa,” alisema Zitto.
Alisema nafuu ya kodi kwa wafanyakazi nchini katika sekta zote na hasa wafanyakazi wa kima cha chini itachochea matumizi binafsi ya bidhaa na huduma na hivyo kuchangamsha uchumi na kuwezesha uwekaji wa akiba.
“Nashauri ukaguzi zaidi ufanyike katika utumishi wa umma ili kumaliza kabisa tatizo la wafanyakazi hewa.”
Aliipongeza Serikali kwa kuanzisha kodi ya zuio ya ada kwa wakurugenzi wa kampuni na mashirika akisema itaongeza mapato ya Serikali.

Related

KIMATAIFA: NDEGE NYINGINE YA MALAYSIA YAPOTEZA MAWASILIANO NA KUANGUKA UKRAINE IKIUA ABIRIA WOTE 295

+42 Crash site: Rescue workers inspect the wreckage of a Malaysia Airlines passenger plane which was shot down today above Ukraine, killed all 295 people on board +42 Destructi...

MATOKEO: MATOKEO YA KIDATO CHA SITA (FVI) MWAKA 2014 YAMETOKA. ANGALIA HAPA NA SHULE ZILIZO ONGOZA

MATOKEO YA KIDATO CHA 6 2014 YATANGAZWA Matokeo ya mtihani wa kidato cha 6 yaliyofanyika tarehe Mei 5 – 21, yametoka.Jumla ya watahiniwa 38,905 sawa na asilimia 95.98 ya watahiniwa waliofany...

KITAIFA: WAZIRI WA MALIASILI AGEUKWA, KAMPUNI YA UWINDAJI KUMFIKISHA MAHAKAMANI KWA TUHUMA NZITO MALIASILI

  UONGOZI wa Kampuni ya Uwindaji wa Kitalii ya Green Mile Safari Ltd (GMS), umesema haukubaliani na uamuzi wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu wa kuwafutia leseni, hivyo wam...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item