jaridahuru

Mitandao

JKT: UTARATIBU WA KUJIUNGA KWA MUJIBU WA SHERIA KWA WALIOMALIZA MEI 2014

AWAMU YA KWANZA; Vijana 20,000 wataripoti kwenye makambi ya mafunzo ya JKT
kuanzia tarehe 01 Juni 2014 na kuanza rasmi mafunzo yao tarehe 08 Juni
2014 na kumaliza tarehe 04 Septemba 2014. Orodha yao itaanza kuonekana
kwenye website ya JKT tarehe 11 Mei 2014 kuanzia saa nne (4)
asubuhi. 
AWAMU  YA PILI; Vijana 14,450 wataripoti kwenye makambi ya mafunzo ya JKT
kuanzia tarehe 11 Septemba 2014 na kuanza rasmi mafunzo tarehe 18
Septemba 2014 na kumaliza tarehe 17 Desemba 2014. Orodha yao itaanza
kuonekana kwenye website ya JKT tarehe 15 Mei 2014 kuanzia saa kumi (10)
jioni.
  • Kijana yeyote mwenye ulemavu unaoonekana aripoiti katika kambi ya mafunzo ya Ruvu JKT (832 Kikosi cha Jeshi).
  • Vijana wote wanatakiwa kuwa na vyeti vya kumaliza Kidato cha Sita (Leaving Certificate).
  • Inasisitizwa vijana waripoti kwenye makambi waliyopangiwa na siyo kuja Makao Makuu ya JKT.
Bofya majina ya makambi yaliyopachikwa hapo chini kupakua na kufungua ukurasa kuona majina ya walioitwa katika Awamu ya Kwanza.
  1. BULOMBORA - KIGOMA
  2. RWAMKOMA - MUSOMA
  3. MSANGE - TABORA
  4. KANEMBWA - KIGOMA
  5. RUVU - PWANI
  6. OLIJORO - ARUSHA
  7. MGAMBO KABUKU - TANGA
  8. MARAMBA - TANGA
  9. MAFINGA - IRINGA
  10. MLALE - SONGEA
  11. MTABILA - KIGOMA
  12. MAKUTOPORA - DODOMA
Kwa ufafanuzi zaidi wasiliana na info@jkt.go.tz

Taarifa hii imetolewa na:
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa.



Related

Vyuoni 6789844842291624555

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item