jaridahuru

Mitandao

JH STORY: UTAOA LINI BWANA?!



UTAONA LINI...



2008, January 28 Jumatatu
Ndo nilikuwa natimiza miaka 26. Kijana mtanashati miaka miwili kazini katika kampuni moja ya vinywaji.
Siku hii bosi wangu alinipa ofa ya a whole crate ya vinywaji..my fellow workers wakaorganize surprise bash for me. Kwa kweli sikuwa nimeitegema kwani birthday yako ikiangukia Jumatatu (kama ya mwaka huu) huwa huna plan yoyote kubwa since unajua the following day ni kazini!

Nilipotoka kazini mshkaji akanipigia simu;
Mike: “Oya Mentor upo wapi?”
Me: “Dah ndo natoka job mtu wangu naenda home tu”
Mike: “Aaah pitia hapa NISIKUONE NA MWANANGU pub bana kuna mshkaji anasema anajua biometric readers vizuri labda anaweza kukusaidia project yako”
Me: “Mh Mike, hatuwezi kutana weekend?”
Mike: “mshkaji mwenyewe si wa kukaa sana ka vipi pitia tu si ndo njia hiyohiyo ya kwenda home mwana?”
Basi bana mbele ya teknolojia? Ikabidi na uchovu wangu nijikongoje hadi pale.


NISIKUONE NA MWANANGU Pub, 1830hrs
Ile naingia tu..nasikia SUUURPRIIISEEE!!! Ndo nikashtuka aaah kumbe its my birthday…I was really surprised kwa kweli but delighted as well...We really drank that night.

Something extraordinary happened…I met a girl.

A very beautiful lady. 23 yrs was her age. A finalist at Muhimbili.

Namimi kwa courage ya birthday boy nikamfuata nikaomba kudance naye. Ofcourse alikubali…haha

Basi kidogo kidogo tukaanza kupiga stori za hapa na pale na hata muziki ulipoisha tukaenda pembeni kuendeleza stori.
Aliniambia kuwa alikuja pale na dada yake ambaye ni co-worker wangu. Basi nikachukua contacts zake tukawa tunaendelea kuwasiliana.

To cut the long story short…
Kidogo kidogo tulizoeana na ilichukua two months tu kuhakikisha amekuwa wangu. Alionesha kunipenda kwa dhati na hata alipomaliza chuo nilimwambia nataka kuanza michakato ya kumfanya awe mke wangu. Alinijibu sentensi ambayo kwa kipindi kile sikulitilia maanani, “Hilo tulishalijua!”

Basi michakato ya kwenda kwao ilianza nikamtumia mshkaji wangu Mike koz alikuwa amenizidi anisaidie kufanya hiyo michakato ifane. Kama kupeleka barua na formalities nyingine.

Nilimvalisha pete (ambayo alisisitiza aichague yeye…kwenye duka specific) na tukawa tunasubiri siku ya harusi tu tuhalalishe mambo.

2010 January 23 Jumamosi
Alikuja kwangu Ijumaa. Tukaenda kuangalia live band ya kina Hamis Mwinjuma…then ikabidi aje kulala kwangu aondoke asubuhi awahi kazini kwani ni nesi na alikuwa zamu siku hiyo.

Basi kwa haraka ya kuwahi job akasahahu simu yake kwangu.
Mida kama ya saa tatu hivi ndo nashtuka kusikia inaita…alikuwa akipiga shoga ake mmoja ivi. Iliita kama mara tatu ikanibidi niipokee tu.

Nikapokea;
Shosti: “We mwanga wa kike nikipiga mimi unajifanya upo na jianaume lako ambalo kama sio mimi usingelipata. Muone kwanza na leo nina maagizo toka kwa mganga wako nimeamua nikuambie kwa mdomo si unajifanya kusoma message hujui!

Ilinibidi nikate simu kwa mshtuko…curiosity got the best of me ikanibidi niingie ndani ya simu ambayo kwa muda wote wa mahusiano yetu sikuwahi kuigusa. Nakumbuka kuna kipindi niliishiwa credits ghafla ikabidi nimuombe nimpigie mshkaji akanitaka nitaje namba aandike mwenyewe na nilipomaliza akataka kukata mwenyewe.

Nikazama kwenye messages…
Nilishtuka sana siku ile. Sikujua kama haya mambo bado yapo…ya kwenda kwa waganga? Binti mrembo vile? Na kanisani mbona alikuwa anaenda? Na usomi wake je?..nilijiuliza mambo mengi sana nikakosa jibu..

: kulikuwa na masharti ya kuhakikisha ananipata na ninakuwa mumewe kwa hali yoyote ile
: kulikuwa na masharti ya kuhakikisha anapata pesa kama kuvaa chupi kwa mwezi
:kulikuwa na masharti ya kuendesha gari bila kuvaa chupi
:masharti ya kulala juu ya kaburi (hizi ni siku aliniambia anaenda safari za kikazi)

I have been single since then…
 
Here i sign-out!
Sebastian.

By Sebastian

Related

Mahusiano 572611170351407148

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item