KIMATAIFA: RAIS OBAMA ATANGAZA KUPANUA WIGO VIKWAZO DHIDI YA URUSI
https://jaridahuru.blogspot.com/2014/07/kimataifa-rais-obama-atangaza-kupanua.html
Rais Barack Obama wa Marekani ametangaza kupanua
uwigo wa vikwazo dhidi ya Urusi kufuatia mgogoro unaoendelea
Ukraines.Tangazo hilo la Rais Obama linafuatia vikwazo vilivyotangazwa
na Jumuiya ya Ulaya saa chache kabla ya hili la Marekani.
Vikwazo hivyo vilivyotangazwa Marekani imesema itaiwekea vikwazo Urusi katika maeneo ya nishati,silaha na uchumi.
Hata hivyo Rais Obama amekanusha madai kwamba
vikwazo hivyo vyaweza kuanzisha vita baridi dhidi ya Urusi, bali amesema
kuwa wanalenga kuhakikisha Ukraine inarejea katika hali yake na
kufuatia machafuko yanayoendelea hivi sasa.