jaridahuru

Mitandao

KIMATAIFA: JESHI LA WANANCHI ITALIA LAPATA MAITI 30 ZINAZODHANIWA KUWA ZA WAHAMIAJI HARAMU UFUKWENI



Jeshi la wanamaji nchini Italia , limepata maiti 30 katika mashua ya uvuvi ambayo ilikuwa imewabeba mamia ya wahamiaji haramu.

Mashua hiyo ilipatikana katika eneo moja lililo kati ya mji wa Siciliy nchini Italia na Kaskazini mwa pwani ya Afrika.




Wahamiaji waliofariki walisemekana kufariki kutokana na kukosa hewa.

Ugunduzi huo ulifanyika wakati waokoaji walipotumia mashua hiyo kutaka kuokoa idadi kubwa ya watu waliosemekana kuwa katika hali ngumu baharini.

Miongoni mwa watu hao walikuwa wanawake wawili wajawazito.
Wanajeshi hao walisema kuwa mwishoni mwa wiki waliwaokoa zaidi ya watu hamsini waliokuwa wanajaribu kuvuka na kuingia Italia kutoka Kaskazini mwa Afrika.

Jeshi la wanamaji la Italia

Idadi hiyo ya wahamiaji ilitolewa baada ya habari kutolewa kuhusu maiti zilizopatikana.
Wanajeshi hao walisema kuwa watu waliofariki, walifariki kuokana na kukosa hewa kwani walikuwa katika sehemu ya chini ya mashua hiyo.

Mashua hiyo ilikuwa imewabeba takriban wahamiaji 600.
Mkasa wa huo unaonyesha hatari inayowakumba watu wanaotumia kila njia kufika barani ulaya ikiwemo kutumia vyombo ambavyo ni tishio kwa maisha yao.

Italia kwa mara nyengine imesema kuwa mataifa mengine ya ulaya hayafanyi lolote ili kulisaidia taifa hilo kuzuia maafa kama hayo.

Related

Kimataifa 5970108810867012799

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item