jaridahuru

Mitandao

MATUKIO: WANANCHI WAVUNJA MOCHUARI KUTAKA KUONA MAITI



Muleba. Polisi wamelazimika kutumia mabomu ya machozi kutawanya baadhi ya wanakijiji wa Bukono, Kata ya Muleba, mkoani Kagera ambao walivunja mlango wa chumba cha kuhifadhi maiti Kituo cha Afya Kaigara, wakitaka kuchukua maiti ya mtoto aliyefariki dunia mkoani Arusha alikokuwa akifanya kazi za ndani.

Mtoto huyo Asela Triphone (16) alikuwa akifanya kazi za ndani kwa mwanamke mmoja aliyemchukua kutoka kwa wazazi wake.

Wanakijiji hao walichukua hatua hiyo, wakidai mwili uliokuwa kwenye jeneza ulikuwa umenyofolewa baadhi ya viungo vya mwili; sehemu za siri, mkono na mguu ikidaiwa kuwa vilichukuliwa kwa ajili ya imani za kishirikina.

Inadaiwa kuwa baada ya kufika Arusha, Asela alianza kufanya kazi za ndani na alifariki dunia katika mazingira ya kutatanisha na mwili wake ulirejeshwa juzi kwa wazazi wake.

Akisimulia tukio hilo, mama wa marehemu, Georgina Triphone alisema aliombwa mtoto wake kwenda kufanya kazi za ndani Januari mwaka jana na kwamba, alikuwa akipata mawasiliano ya simu kutoka kwa mwajiri wake.

“Tangu Alhamisi (Juni 12, mwaka huu), nimekuwa nikipokea simu tofautitofauti kuhusu binti yangu kupitia kwa mwajiri wake kuwa, atakuja karibuni kusalimia,” alisema na kuongeza: “Ijumaa (Juni 13 mwaka huu), nilipigiwa simu na mwajiri wa binti yangu kuwa, angekuja kuwatembelea lakini kesho yake alinitaarifu kuwa ni mgonjwa na Jumapili nikaletewa maiti ya binti yangu.”

Alisema yeye na mumewe walianza kujawa na wasiwasi juu ya binti yao na jeneza lilipowasili walitaka kulifungua lakini walikatazwa na aliyefika na maiti hiyo kwa madai kuwa mwili ulikuwa umeharibika.

“Tulipokuwa tunalazimisha kuona mwili tuliambiwa ugonjwa uliosababisha kifo chake unaambukiza, hivyo ungeweza kuwaathiri wananchi waliokuwapo.”

Hata hivyo, baba wa marehemu Triphone Basheka alisema mwili huo ulikuwa umeunguzwa sehemu mbalimbali na kwamba, wananchi walitaka kujua ukweli huo baada ya kukosa ushirikiano wa madaktari na vyombo vya dola ikiwamo Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya.

Hatua hiyo iliwakera wananchi ambao walianza vurugu, hali iliyosababisha polisi kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya huku baadhi yao wakikamatwa.

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Muleba, Lambris Kipuyo alikanusha taarifa ya kwamba Kamati ya Ulinzi na Usalama haikutoa ushirikiano na kukemea tabia ya wananchi kujichukulia sheria mkononi.

Kipuyo alisema kwa mujibu wa uchunguzi, viungo vinavyodaiwa kunyofolewa vilikuwapo na kilichosababisha utata ni kukosekana kwa meno manne na mwili kuwa na makovu mbalimbali.

Related

Events 3008140713440707163

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item