jaridahuru

Mitandao

KITAIFA: LOWASSA AIBUKA NA MSIMAMO MPYA, AIZUIA JWTZ KUCHUKUA ARDHI YA WANANCHI, AWAPA SIKU 7 TU KUIRUDISHA

Mbunge wa monduli na waziri mkuu mstaafu. Mhe. Edward Lowassa
Monduli. Waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa ameipa wiki moja Halmashauri ya Wilaya ya Monduli kuzipatia ardhi kaya 63 za Kijiji cha Nanja, ambazo zimetakiwa kupisha eneo la Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wilayani hapa.
Akizungumza katika uzinduzi wa Bwawa la Migwara lililojengwa upya na kampuni ya Ms Meero Contractors kwa thamani ya Sh870.1 milioni. Lowassa ambaye ni mbunge wa jimbo hilo, alisema wananchi hao wanapaswa kuhamishiwa katika shamba lililokuwa la mwekezaji la Oguru ambalo sasa linamilikiwa na halmashauri.
Alisema sambamba na mifugo yao, wanapaswa kuhamia katika eneo hilo kabla ya mwezi huu, kwani tayari Halmashauri ya Monduli ilishafanya uamuzi wa kuwapa ardhi hiyo zaidi ya miaka miwili iliyopita, lakini suala hilo halijatekelezwa.
“Halmashauri ya Monduli ina madiwani wengi vijana, lakini cha ajabu wanafanya kazi taratibu kama konokono. Tukifanya uamuzi inachukua muda mrefu kutekelezwa, tulishaamua Shamba la Oguru litakaliwa na familia 63 za Nanja na mifugo yao,” alisema Lowassa.
Alisema wakati halmashauri hiyo ikiwa inatekeleza mpango wa kuwanyang’anya wawekezaji mashamba 43 waliyoyatelekeza, yale ambayo tayari yapo mikononi mwa halmashauri wayagawe kwa wananchi.

Related

Kitaifa 9175391238773742934

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item