KIMATAIFA: TAASISI YA AFYA YASHAMBULIWA KWA BOMU NCHINI NIGERIA, KADHAA WAJERUHIWA
https://jaridahuru.blogspot.com/2014/06/kimataifa-taasisi-ya-afya-yashambuliwa.html
Mlipuko umeripotiwa kutokea katika taasisi moja ya
umma ya mafunzo ya afya katika mji wa Kano ambao ni wa pili kwa ukubwa
nchini Nigeria.
Mji huo umewahi kulengwa na wapiganaji wa kiisilamu wa Boko Haram, ambao wanataka kubuniwe taifa la kiisilamu Kaskazini mwa Nigeria.
Majimbo matatu Kaskazini mwa Nigeria bado yapo chini ya sheria ya hali ya hatari kufuatia miaka mingi ya harakati za wapiganaji hao wa kiisilamu.