JAMII: AJALI MBAYA YATOKEA HUKO MAKONGO JIJINI DAR, 6 WAPOTEZA MAISHA. (Tahadhari, Picha zinatisha)
https://jaridahuru.blogspot.com/2014/06/jamii-ajali-mbaya-yatokea-huko-makongo.html
Watu
kadhaa wameripotiwa kufariki Dunia kwenye ajali mbaya iliyohusisha
magari matatu ikiwemo lori la mchanga huku mawili yakiwa ni ya abiria
maarufu kama daladala yanayofanya safari zake kati ya ubungo na Tegeta.
Ajali hiyo imetokea mchana kwenye eneo la kikosi cha jeshi
cha Lugalo jijini Dar es salaam. Jeshi la Polisi mkoa wa Kinondoni
limethibitisha kutokea kwa ajali hiyo mbaya iliyosababisha vifo vya watu
6, watatu wakiwa ni wanaume na watatu wakiwa ni wanawake huku hali za
majeruhi ambao walikimbizwa hospitali ya Lugalo zikielezwa kuwa ni
mbaya.
Bado jeshi la Polisi limeendelea na uchunguzi kujua iwapo
dereva wa daladala hiyo lenye nambari za usajili T 377 BEF
aliyesababisha ajali hiyo kama alifanya uzembe ama la.
Habari zilizo tufikia ni kwamba ajali hii mbaya imetokea eneo la
Makongo. Coaster mbili zimegongana watu 20 wamefariki hapo hapo.
R.I.P