jaridahuru

Mitandao

KIMATAIFA: SUDANI KUSINI WAKIUKA SAINI YA MAKUBALIANO YA AMANI WAINGIA VITANI TENA


Saa chache tu baada ya kutiwa saini kwa mkataba wa usitishaji mapigano nchini Sudan kusini Malumbano yameibuka .

Sasa Serikali na wapiganaji wa Sudan Kusini wanalaumiana kila upande ukimshutumu mwenzake kuvunja makubaliano hayo yaliyosainiwa ijumaa.

Hata hivyo kiongozi wa waasi Riek Machar anasema bado ameazimia kutekeleza makubaliano hayo licha ya kwamba anasema serikali ya rais Salva Kiir inavunja mapatano hayo.

Machar amesema kuwa majeshi ya UPDF ya Uganda ambayo yamekuwa yakivamia maeneo inayoyadhibiti haijaafiki mkataba uliotiwa sahihi huko Adiss Ababa kati yake na Rais Salva Kiir.
Aidha msemaji wa jeshi la serikali, Kanali Philip Aguer, amesema waasi hao wameshambulia maeneo ya serikali katika mji wa Bentiu .

Upinzani umepinga madai hayo.
Machar amesema kuwa angetaka mazungumzo zaidi na serikali kuhusu hilo, lakini amesema anafahamu kuwa Rais hana uwezo wa kudhibiti majeshi yote yanayopigana kwa upande mmoja na majeshi ya serikali kama vile majeshi ya Uganda na wapiganaji kutoka Darfur.
Serikali ya Sudan Kusini pia imelaumu upande wa waasi kwa kuvunja makubaliano ya kusitisha mapigano saa chache tuu baada ya mkataba huo kutiwa saini.

Makubaliano ya kusitisha mapigano yalitiwa saini Ijumaa, na yalikusudiwa kumaliza vita vya miezi mitano ambavyo vimeuwa maelfu ya watu na kulazimisha zaidi ya milioni moja kuhama makwao.

Chanzo: BBC

Related

KIMATAIFA: TAHADHARI YA MASHAMBULIZI NCHINI UGANDA, POLISI WATANDA MJI WA KAMPALA

Polisi nchini Uganda wamedhibiti usalama mjini Kampala kufuatia onyo la mashambulizi ya kigaidi kupangwa kufanywa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Entebe. Maafisa wa usalama katika...

KIMATAIFA: JESHI LA WANANCHI ITALIA LAPATA MAITI 30 ZINAZODHANIWA KUWA ZA WAHAMIAJI HARAMU UFUKWENI

Jeshi la wanamaji nchini Italia , limepata maiti 30 katika mashua ya uvuvi ambayo ilikuwa imewabeba mamia ya wahamiaji haramu. Mashua hiyo ilipatikana katika eneo moja lililo kati ya mji wa ...

KIMATAIFA: BOKO HARAM WAZIDI KUITEKETEZA NIGERIA, WASHAMBULIA VIJIJI NA MAKANISA MENGINE TENA

Watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa Boko Haram wameshambulia vijiji kadha na makanisa kaskazini mashariki mwa Nigeria. Wakaazi wa huko walisema kuwa watu wengi wameuwawa na nyumba nyingi zimet...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za JuuMitandaoPiga Kura

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item