jaridahuru

Mitandao

SIASA: WAZIRI WA UJENZI, JOHN MAGUFULI NAE AELEZEA KUHUSU NIA YAKE YA KUGOMBEA URAIS 2015




WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, amesema kuwa hana mpango na urais wala kujitangaza kuwania nafasi hiyo.

Hatua hiyo ilitokana na wananchi wengi kumshangilia na kumwita rais wakati ziara ya siku tatu ya kukagua miradi ya ujenzi wa barabara, madaraja na vivuko.

Akiwa katika eneo la Tegeta, aliwaeleza wananchi kazi ambazo serikali imekuwa ikizifanya katika kuhakikisha inaondoa adha ya foleni jijini Dar es Salaam ambapo wakimshangilia na kumpatia sifa za kuwa rais 2015.

Hata hivyo, Dk. Magufuli alikanausha habari hizo na kueleza kuwa ni maono ya wananchi na si yeye.
“Sina mpango huo nipo katika ziara kuangalia utendaji wa watu tuliowapatia kazi, hayo ni maono yao,”alisema.

Magufuli anaonekana kuwa tofauti na baadhi ya vigogo wa CCM ambao kwa nyakati tofauti wamekuwa wakijinadi kuusaka urais.

Related

Siasa 255934160620319504

Post a Comment

emo-but-icon

Wadhamini

UJUMBE

JH Katika Facebook

Nyayo zetu twitter

Za Juu

Mitandao

Piga Kura

Je ungependa Tanzania iwe na serikali ngapi?
  
pollcode.com free polls 

ADVERTISEMENTS

Msimamo wa ligi mbalimbali

Football results provided by whatsthescore.com

Mechi Live

Walioko Hewani Kwa Sasa

item